Man United kusajili nyota wapya watatu au wanne .

Mabingwa wa taji la Europa ligi msimu huu klabu ya Manchester United inatarajiwa kuweka kikomo cha kufanya usajili kwa wachezaji watatu au wanne muhimu katika dirisha kubwa la usajili
Meneja wa United Jose Mourinho amesema makamu mwenyekiti wa timu hiyo Ed Woodward anajua wachezaji wanaotakiwa kwa zaidi ya miezi miwili iliyopita.
"Ed Woodward anayolisti yangu ya wachezaji ninaowataka ," alisema meneja huyo baada ya mchezo wa Europa ligi dhidi ya Ajax .
Mourinho anataka kuongeza changamoto katika safu ya ulinzi na ushambuliaji ili kuweza kuwania taji la ligi kuu ya England msimu ujao.
United wamekua wakihushwa na kutaka kuimarisha safu ya ushambuliaji kwa kuwasajili Antoine Griezmann toka Atletico Madrid, Andrea Belotti wa Torino pamoja Romelu Lukaku.
Kwa Upande wa safu ya ulinzi wachezaji wanaotajwa kuwa wako kwenye rada ya Mourinho ni beki wao wa zamani Michael Keane anayechezea Burnley,beki kisiki wa Benfica Victor Lindelof na Muholanzi Virgil van. Dijk wa Southampton.

Comments


Popular posts from this blog

DROO YA KLABU BINGWA ULAYA HII HAPA

Nyumba ya Mbunge Kigoma Mjini Zitto Kabwe yaungua moto

Wanawake wasiowaita waume kwa majina yao India

Cristiano Ronaldo kawaonesha watoto wake mapacha leo

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO

Baada ya Kifo cha Mumewe… Zari Akwaa Aibu 5 #Tazama

hali ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu

Emmanuel Mbasha, aweka wazi haya .