Ndemla sasa shavu dodo

Meneja wa mchezaji huyo wa Simba na timu ya taifa ya Tanzania, Jamal Kisongo amesema kuwa ni kweli Ndemla amepata nafasi hiyo lakini kikwazo kikubwa kwa sasa ni Visa ya kuingia na kufanya kazi nchini Sweden ndiyo ambayo bado inasumbua.
Kisongo amesema kuwa Ndemla amefuzu majaribio yake ambayo alienda mara ya kwanza na wao wapo kwenye mchakato wa kutafuta Visa ya kumwezesha kukamilisha uhamisho wake ili akacheze soka la kulipwa.
“Bado suala la Visa ni tatizo lakini tunalifanyia kazi, Ndemla ni mchezaji mzuri na mimi ni mmoja wa mashabiki wake, amekuwa akionyesha uwezo mzuri uwanjani.
“Kuhusu suala lake tutaenda TFF wakatusaidie, nitamfuata katibu wa TFF atusaidie juu ya suala hilo na pia serikali inaweza kuingilia kusaidia ili kufanikisha mchakato wa kupata vibali, unajua timu ambayo anatakiwa kwenda Ndemla ni ile ambayo alikuwa akiichezea Thomas Ulimwengu.”

Comments


Popular posts from this blog

ILE SINTOFAHAMU YA NANI BINGWA WA VPL HII HAPA

Michezo:Ajibu huyo yanga

ELIZABETH MICHAEL ' LULU' awafungukia wasanii wa bongo move

fahamu kilichojiri nyumbani kwa Tundulisu