Posts

Showing posts from September, 2017

CCM wafuta uchaguzi wilaya nne

Image
Uamuzi huo umetangazwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole baada ya mkutano huo ambapo amezitaja wilaya hizo zilizofutiwa uchaguzi kwamba ni Moshi Mjini,  Siha, Hai, pamoja na Makete. Amesema sababu ya kufuta matokeo hayo ni kubainika kwamba wagombea waliojitokea hawakuwa na sifa, pamoja na kubainika kuwepo na viashiria hatarishi kwa chama na kuwa halmashauri imetaka kuanza upya kwa utaratibu wa kupata wagombea wapya   Na eatv

ushahidi madiwani waliojiuzulu kuanika

Image
Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amesema kesho Jumapili ataweka hadharani ushahidi wa tuhuma walizonazo kuhusu madiwani wa chama hicho waliojiuzulu wakisema ni kutokana na kuunga mkono utendaji wa Rais John Magufuli. Lema na mbunge mwenzake wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari wamewatuhumu madiwani hao wakisema uamuzi wao unatokana na rushwa. Hata hivyo, madiwani hao kwa nyakati tofauti wamekuwa wakikanusha tuhuma hizo. Lema akizungumza na Mwananchi leo Jumamosi, amesema wataweka hadharani ushahidi huo kesho kabla ya Jumatatu kuupeleka kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).  Na mwananchi

Mahakama imetoa siku 14 kwa serikali

Image
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam imetoa siku 14 kuanzia leo mshtakiwa Harbinder Sethi akatibiwe katika Hospitali ya Taifa Muhimbili maradhi yanayomkabili na kinyume cha hapo itamuita Mkuu wa Magereza kumuhoji kuhusiana na hilo.Amri hiyo ya Mahakama imetolewa baada ya Wakili wa serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa kudai kesi hiyo ilipangwa kusikilizwa leo (Ijumaa) lakini upelelezi haujakamilika na kuomba shauri lipangiwe tarehe nyingine. Kutokana na hayo kesi imeahirishwa na kusikilizwa tena hadi Oktoba 13, 2017. Mfanyabiashara Harbinder Sethi anatuhumiwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi pamoja na utakatishaji fedha na kuisababishia serikali kuingia hasara.  Na eatv

Diamond Platnumz aweka Rekodi mpya

Image
Staa wa Bongo Fleva kutoka Tanzania Diamond Platnumz amefanikiwa kuweka Rekodi mpya ya Watazamaji wa video za wasanii kwenye mtandao wa Youtube baada ya video yake kutazamwa na watu zaidi ya Milioni 1 ndani ya Masaa 15. Hii video ya Diamond

video mpya ya Madee Ft Nandy ‘Sema’ Itazame

Image
video mpya ya Madee Ft Nandy ‘Sema’ Itazame Hapa Hii a

Magazeti ya Tanzania leo September 30 2017 kuanzia ya Udaku, Michezo na Hardnews

Image
Ni asubuhi nyingine tena nakukutanisha na habari kubwa kwenye Magazeti ya Tanzania leo September 30 2017 kua nzia ya Udaku, Michezo na Hardnews kujionea yote makubwa yaliyoandikwa

Mara paa Barcelona kucheza Ligi Kuu England EPL

Image
Uwezekano wa Barcelona kucheza Ligi Kuu England utaongezeaka iwapo mchakato wa kudai uhuru Catalan utapitishwa kesho kutwa Jumapili. Barcelona ikijitoa tu Jimbo la Catalonia, kuhamia Ligi Kuu England Wizara ya Michezo nchini Hispania imesisitiza kwamba klabu ya Barcelona itapoteza sifa ya kucheza Ligi Kuu ya nchini humo maarufu La Liga iwapo Jimbo la Catalonia litajitenga na kuwa nchi huru. Uwezekano wa Barcelona kucheza Ligi Kuu England utaongezeaka iwapo mchakato wa kudai uhuru Catalan utapitishwa kesho kutwa Jumapili. Waziri wa Michezo nchini humo alidokeza kuwa iwapo mabadiliko hayo yatapitishwa jambo hilo litakuwa halikwepeki. Hata hivyo taarifa zaidi zinasema kwamba Serikali ya Hispania imetangaza kutoruhusu kupigwa kura hiyo ya mabadiliko, huku polisi ikidhibiti masanduku ya kura. Pia Waziri Mkuu wa nchi hiyo amesema kwamba hakuna mchakato wa mabadiliko utakaofanyika nchini humo. Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola amekuwa miongoni mwa watu wanaounga mkono Jimbo l

Bashe apingana na Msemaji wa Serikali

Image
Hussein Bashe alitumia mtandao wake wa Twitter pia kujibu hoja juu ya kauli ya Msemaji wa Serikali na kusema kuwa neno 'Usalama wa Nchi' muda mwingine linatumika vibaya kwa ajili ya kulinda utashi wa watu waliopo madarakani. " Usalama wa Nchi" muda mwingine neno hili hutumika vibaya kulinda Utashi wetu sisi watawala . Ni vizuri kuwapa watu nafasi ya kupumua" aliandika Hussein Bashe Jana baadhi ya viongozi wa serikali walikutana na wadau mbalimbali ambao walikuwa wakitoa maoni yao ili kuboresha kanuni za maudhui ya Utangazaji na Mitandao ya Kijamii ambapo Katibu Mkuu Wizara Habari Prof. Elisante ole Gabriel alisema kuwa mitandao ya kijamii inatoa habari kwa haraka na kusema mfumo wa sasa wa mitandao ya kijami unachangia kutoa taarifa za uongo, chuki na hata kuhatarisha usalama wa nchi.

Nyumba yamuwekezaji kuvunjwa

Image
Naibu Waziri huyo alitoa, agizo hilo leo alipokuwa ametembelea shamba la mpunga la kilimo cha ushirika Ruvu (CHAURU) ambapo alielezwa kuwa kuna mgogoro kati ya wakulima na mwekezaji wa kichina aitwaye Guo Ming Tang ambaye aliingia mkataba batili na uongozi wa awali wa ushirika huo mwaka 2012 kwa niaba ya CHAURU. Mwenyekiti wa CHAURU, Sadala Chacha amemweleza Naibu Waziri kuwa mgogoro huo umekuwa wa muda mrefu na kuwa kuziba mfereji huo kumesababisha ekari 24 kutokulimika kwa miaka mitano na kusababisha upotevu wa wastani wa kilo 236,000 za mpunga zenye thamani ya sh. 200,600,000. Baada ya kuelezwa migogoro kadhaa kati ya wakulima na mwekezaji huyo, ikiwemo huo wa kuziba mfereji na pia kuwauzia maji wakulima,ya kumwagilia kwa saa moja kwa bei ya sh. Laki moja naibu waziri alitoa maagizo kadhaaa sambamba na kuvunjwa kwa nyumba hiyo ya mwekezaji.  Na eatv

Diamondameamua kuachia video nyingine mpya ya wimbo wa “Hallelujah” itazame hapa

Image
Leo September 29 2017 ameamua kuachia video nyingine mpya ya wimbo wa “Hallelujah” ambao amemshirikisha Morgan Heritage… ndio hii hapa chinichini T l

Meya Boniface Jakob afunguka mazito

Image
Meya Boniface Jakob amedai Makonda amemtafuta akitaka wamalizane, jambo ambalo analitafriri kama vitisho. Meya huyo pia amesema ushahidi wote alioupeleka kwenye shauri hilo, haujapingwa mpaka sasa. Pia amesema ameambiwa na Makonda afute hiyo kesi kwa kuwa naye alikiuka maadili kwa kufanyia vikao vya chama kwenye ofisi yake ya Meya Amejibu hilo na kusema yeye hakufanyia kikao cha chama ofisini ila alitembelewa na Sumaye ofisini. Na akahoji mbona Magufuli anafanyia vikao vya CCM Ikulu? Akasema sekretarieti ya maadili ya viongozi wa uma itaheshimika milele au itadharaulika milele kulingana na maamuzi watakayofanya juu ya swala hilo. Amesema pia lengo lake sio kumdhalilisha au kumfanya asiwe mkuu wa mkoa ila kuweka rekodi sawa kuwa amefoji vyeti. Na wanaopinga kuwa anamfungulia kesi wakati Dar ina matatizo lukuki, anahoji mbona kuna watu waliokuwa wanakaribia kustaafu wamefukuzwa kazi na mafao yao yamegubikwa na utata?

Hiki ndicho kilichomkuta Freeman Mbowe

Image
Mkuu wa idara ya Uenezi CHADEMA, Hemedi Ali amefunguka na kusema gari ambayo Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe alipewa na Bunge kwa ajili ya mizunguko mbalimbali ambayo pia ilikuwa akiitumia Nairobi kwenye matibabu ya Lissu imenyang'anywa na Bunge Akiongea kutokea Nairobi, Hemedi Ali amesema kuwa haoni dhamira ya dhati ya Bunge hilo kusema lipo tayari kumtibu Tundu Lissu ikiwa wamepokonya gari ambayo Kiongozi wa Kambi rasmi Bungeni alikuwa akiitumia Nairobi kwenye matibabu ya Tundu Lissu.

mikutano ya Godbless Lema yazuiwa

Image
Polisi Wilaya ya Arusha imepiga marufuku mikutano ya hadhara ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kwa maelezo kuwa kutakuwa na ujio wa viongozi wa kitaifa jijini hapa. Pia, kuzuiwa mikutano ya mbunge huyo wa Chadema kunahusishwa na tukio la kuungua moto nyumba za polisi. Katika barua ya Mkuu wa Polisi Wilaya ya Arusha, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP E.Tille kwenda wa Lema  Jumatano, imeeleza mikutano yake imesitishwa. Mikutano hiyo ilikuwa ifanyike leo Alhamisi na kesho. Katika barua hiyo, Jeshi la Polisi limeeleza kuwa tarehe ambazo mikutano hiyo, imepangwa zina mwingiliano na ratiba za shughuli za kiserikali za viongozi wa juu wa Serikali inayoishia Oktoba 4. Pia, amesema janga la moto katika kambi ya polisi lililotokea jana usiku limeleta madhara makubwa hivyo, nguvu kubwa itaelekewa huko. "Unashauriwa kupanga mikutano yako tarehe yoyote kuanzia Oktoba 5, 2017 pia rejea mazungumzo yangu na wewe ofisini kwangu ya tarehe 29/09/2017," inasomeka barua hiyo. Hat

Magazeti ya Tanzania leo September 29 2017 kuanzia ya Udaku, Michezo na Hardnews

Image
Ni asubuhi nyingine tena nakukutanisha na habari kubwa kwenye Magazeti ya Tanzania leo September 29 201 7  kuanzia ya Udaku, Michezo na Hardnews kujionea yote makubwa yaliyoandikwa   Magazeti,

Yanga SC kuzindua uwanja

Image
Uwanja huo ambao umefungwa kwa muda ili kupisha matengenezo yaendelee, na utakapofunguliwa utatumika kama dimba la nyumbani kwa timu ya Singida United ambayo kwa sasa inatumia uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma katika michuano inayoendelea ya ligi licha ya makazi yake kuwa mkoani Singida. Akizungumza Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba ambaye ndiye mdau mkubwa katika matengenezo hayo, amewahakikishia wapenzi wa kandanda mkoani humo kuwa uwanja huo utakuwa tayari kabla ya Novemba 4, 2017 na kuwataka wakazi wa Singida kujiandaa kuishangilia timu yao. Kwa mujibu wa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Singida United imeweza kushika nafasi ya tatu kwa alama tisa ikiwa mbele kwa alama moja dhidi ya Yanga SC ambayo imeshika nafasi ya sita kwa pointi nane.  Na eatv

DPP akwamisha kesi ya Maxence Melo

Image
Kesi ya kuzuia Polisi kufanya uchunguzi, inayomkabili Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jamii Forum, Maxence Melo (40) na Mwanahisa wa mtandao huo, Mike Mushi, imeshindwa kuendelea baada ya upande wa mashtaka kuwasilisha ombi la kuifanyia marekebisho hati ya mashtaka. Kesi hiyo namba 456 ya mwaka 2016, iliyopo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jana ilipaswa kuendelea na ushahidi wa upande wa mashtaka. Wakili wa Serikali, Mutalemwa Kishenyi alimweleza Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba anayeisikiliza kesi hiyo kuwa, ilikuja kwa ajili ya kuendelea na ushahidi lakini wanaomba kuifanyia marekebisho hati ya mashtaka chini ya kifungu 234 (1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA). Hata hivyo, Wakili wa utetezi, Jeremiah Mtobesya alipinga maombi hayo ya kutaka kufanyia marekebisho ya hati hiyo, akidai kuwa tayari mahakama imeshasikiliza shahidi mmoja wa upande wa mashtaka. “Tunaomba mahakama isikubali upande wa mashtaka kubadilisha hati ya mashtaka kwa sababu hatujaambiwa i

Mwigulu Nchemba Wasiojulikana dakika zao zinahesabika

Image
Baada ya kuibuka matukio mbalimbali ya uhalifu nchini na baadhi ya watu kushambuliwa kwa risasi akiwemo Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu na taarifa zikidai wahalifu hao hawajulikani, Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba amesema watu hao dakika zao zinahesabika. Waziri Nchemba akiwa Singida amesema kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha ilinda usalama wa Wananchi na kuwa wahalifu wanaotekeleza matukio hayo wameshindwa tayari.

, Mohammed Dewji nimechelewa

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mohammed Enterprises (MeTL Group), Mohammed Dewji ametaja mambo mawili ambayo anayajutia kwa kutoyafanya na anahisi kuwa amechelewa kuyafanyia maamuzi. Dewji ambaye kwa mujibu wa jarida la Forbes anashika nafasi ya 21 kwa watu matajiri Afrika amesema kuwa kushindwa kuwekeza katika benki na mawasiliano ya simu ni mambo ambayo yanamuumiza kichwa akiendelea kuyajutia. Mfanyabiashara huyo ametuma sehemu ya mahojiano kwenye mtandao wake wa Twitter akielezea mambo hayo. Akijibu swali lililotaka atoe ushauri wake nini ambacho hajakifanya Dewji alianza kwa kusema, “Nimekosa mambo mengi katika maeneo ambayo nilipaswa kuwekeza...nilipaswa nimewekeza katika benki. Ingawa sasa najaribu kununua benki lakini nadhani nimechelewa. Na jambo la pili ambako nimekosea ni kwa kushindwa kuwekeza katika biashara ya mawasiliano ya simu.” Amesema hakuwa na mwamko wa kujiingiza katika uwekezaji wa mtandao wa mawasiliano ya simu kwa vile alihisi wananchi wengi walikuwa ha