Mwezi Mtukufu… Roma Awafuturisha Watoto Yatima
Mkali wa muziki wa Hip Hop Bongo, Ibrahimu Musa ‘Roma Mkatoriki, baada ya juzi kuibukia Shule ya Mchikichini iliyopo Mbagala Rangi Tatu, jana Ijumaa Juni 16 mkali huyo alifuturu na watoto yatima katika kituo cha Dira kilichopo mitaa ya kwa Mzungu Mbagala Jijini Dar. Akizungumza na Global TV Online, Roma alisema aumuzi wa kwenda kufuturu na watoto yatima katika kituo hicho umekuja baada ya kuona ana kila sababu ya Kuungana na watoto yatima na kuwatia moyo katika maisha yao kuelekea kilele ya siku ya watoto duniani. “Tuko katika maadhimisho ya siku ya watoto ulimwenguni, kimisingi nimefurahi kufuturu pamoja na watoto yatima wa kituo hiki. “Lakini pia nimepata nafasi ya kuwatia moyo na kuzungumza nao mambo mbalimbli kuhusu maisha, watoto pia wamefurahi kuniona na wamepata fursa ya kuniuliza mambo mengi. “Nimeambiwa kuna changamoto nyingi hapa kituoni, nimewahidi nitafanya kila liwezekanalo kuhakikisha changamoto zile tunazimaliza siku za hivi karibuni kwa kushirikiana na wasani...


Comments