Kenyata sina matakwa yoyote kutoka IEBC
Katika majadiliano hayo Rais Uhuru amesema yuko tayari kwa uchaguzi na hana matakwa yoyote kutoka IEBC, zaidi ya chombo hicho kutekeleza wajibu wake wa kusimamia uchaguzi mpya wa raia Oktoba 26 kama ulivyoamriwa na Mahakama ya Juu.
Kikao hicho kilifanyika katika Jengo la Harambee, ambako imo ofisi ya Rais katikati ya jiji na kilihudhuriwa pia na Makamu wa Rais William Ruto.
“Tuliweka wazi kwamba hatuna matakwa au masharti kuhusu suala hili. Tumetenga fedha kwa ajili ya IEBC kufanya kazi yake. Sasa watekeleze wajibu wao,” alisema Rais.
“Tunasisitiza kwamba uchaguzi ufanyike Oktoba 26, muda uliopangwa na IEBC kama masharti baada ya uchaguzi wa Agosti 8 kufutwa,” aliongeza.
Septemba Mosi, Mahakama ya Juu ilifuta matokeo ya urais ya Agosti 8 ikidai ilijiridhisha kwamba ulijaa dosari na kukosa uhalali. Tangu wakati huo Rais na makamu wake wamefanya kampeni nzito katika kaunti zote kwa ajili ya uchaguzi huo wa marudio.
Kikao hicho kilifanyika katika Jengo la Harambee, ambako imo ofisi ya Rais katikati ya jiji na kilihudhuriwa pia na Makamu wa Rais William Ruto.
“Tuliweka wazi kwamba hatuna matakwa au masharti kuhusu suala hili. Tumetenga fedha kwa ajili ya IEBC kufanya kazi yake. Sasa watekeleze wajibu wao,” alisema Rais.
“Tunasisitiza kwamba uchaguzi ufanyike Oktoba 26, muda uliopangwa na IEBC kama masharti baada ya uchaguzi wa Agosti 8 kufutwa,” aliongeza.
Septemba Mosi, Mahakama ya Juu ilifuta matokeo ya urais ya Agosti 8 ikidai ilijiridhisha kwamba ulijaa dosari na kukosa uhalali. Tangu wakati huo Rais na makamu wake wamefanya kampeni nzito katika kaunti zote kwa ajili ya uchaguzi huo wa marudio.

Comments