Nyumba yamuwekezaji kuvunjwa

Naibu Waziri huyo alitoa, agizo hilo leo alipokuwa ametembelea shamba la mpunga la kilimo cha ushirika Ruvu (CHAURU) ambapo alielezwa kuwa kuna mgogoro kati ya wakulima na mwekezaji wa kichina aitwaye Guo Ming Tang ambaye aliingia mkataba batili na uongozi wa awali wa ushirika huo mwaka 2012 kwa niaba ya CHAURU.
Mwenyekiti wa CHAURU, Sadala Chacha amemweleza Naibu Waziri kuwa mgogoro huo umekuwa wa muda mrefu na kuwa kuziba mfereji huo kumesababisha ekari 24 kutokulimika kwa miaka mitano na kusababisha upotevu wa wastani wa kilo 236,000 za mpunga zenye thamani ya sh. 200,600,000.
Baada ya kuelezwa migogoro kadhaa kati ya wakulima na mwekezaji huyo, ikiwemo huo wa kuziba mfereji na pia kuwauzia maji wakulima,ya kumwagilia kwa saa moja kwa bei ya sh. Laki moja naibu waziri alitoa maagizo kadhaaa sambamba na kuvunjwa kwa nyumba hiyo ya mwekezaji.

 Na eatv

Comments


Popular posts from this blog

DROO YA KLABU BINGWA ULAYA HII HAPA

Nyumba ya Mbunge Kigoma Mjini Zitto Kabwe yaungua moto

Wanawake wasiowaita waume kwa majina yao India

Cristiano Ronaldo kawaonesha watoto wake mapacha leo

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO

Baada ya Kifo cha Mumewe… Zari Akwaa Aibu 5 #Tazama

hali ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu

Emmanuel Mbasha, aweka wazi haya .