Afisa wa serikali ajinyonga

Kamboi ambaye alikuwa anafanya kazi katika Idara ya Afya kama Afisa Ugavi, aliacha ujumbe akieleza kuwa amepata msongo wa mawazo baada ya kutolewa amri na Gavana wa jimbo hilo, kuchunguzwa iwapo amehusika na vitendo vya uhujumu uchumi, huku akiwataja maafisa wenzake ndiyo waliostahili kubeba msalaba huo.
Kamanda wa Polisi wa jimbo la Nandi nchini Kenya, Peter Wambani amesema marehemu alimuomba mke wake akamuandalie kikombe cha chai huku akiendelea kutazama mpira sebuleni, lakini aliporudi hakumkuta mumewe na baada ya kumtafuta alikuta mwili wake ukining'inia kwenye mti karibu na banda la ng'ombe.
Tukio hilo limetokea huku baadhi ya maafisa wengine wa idara hiyo wamesimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi, kutokana na kupotea kwa fedha za serikali.

  Na eatv

Comments


Popular posts from this blog

wananchi wamshtaki polisi kwakuwanyanyasa

sharti la polepole lapata upinzani

KENYA:Tume Huru ya Uchaguzi yaridhia maombi ya upinzani

Angelina Jolie kuonekana kwenye jarida la ‘Vanity Fair’.

Viongozi wa G7 waangazia bara la Afrika

UEFA kuendelea kutimuavumbi hii leo

YANGA YASHUSHA STRAIKA WA AFCON