Meya Boniface Jakob afunguka mazito

Meya Boniface Jakob amedai Makonda amemtafuta akitaka wamalizane, jambo ambalo analitafriri kama vitisho.
Meya huyo pia amesema ushahidi wote alioupeleka kwenye shauri hilo, haujapingwa mpaka sasa.
Pia amesema ameambiwa na Makonda afute hiyo kesi kwa kuwa naye alikiuka maadili kwa kufanyia vikao vya chama kwenye ofisi yake ya Meya
Amejibu hilo na kusema yeye hakufanyia kikao cha chama ofisini ila alitembelewa na Sumaye ofisini.
Na akahoji mbona Magufuli anafanyia vikao vya CCM Ikulu?
Akasema sekretarieti ya maadili ya viongozi wa uma itaheshimika milele au itadharaulika milele kulingana na maamuzi watakayofanya juu ya swala hilo.
Amesema pia lengo lake sio kumdhalilisha au kumfanya asiwe mkuu wa mkoa ila kuweka rekodi sawa kuwa amefoji vyeti.
Na wanaopinga kuwa anamfungulia kesi wakati Dar ina matatizo lukuki, anahoji mbona kuna watu waliokuwa wanakaribia kustaafu wamefukuzwa kazi na mafao yao yamegubikwa na utata?

Comments


Popular posts from this blog

DROO YA KLABU BINGWA ULAYA HII HAPA

Nyumba ya Mbunge Kigoma Mjini Zitto Kabwe yaungua moto

Cristiano Ronaldo kawaonesha watoto wake mapacha leo

Baada ya Kifo cha Mumewe… Zari Akwaa Aibu 5 #Tazama

hali ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu

Wapiga dili wa madini sasa kukiona

Irine Uwoya: afunguka kuhusu ombi la Dogo Janja kummiliki

hii ndio furaha ya Diamond na zari