Yanga SC kuzindua uwanja

Uwanja huo ambao umefungwa kwa muda ili kupisha matengenezo yaendelee, na utakapofunguliwa utatumika kama dimba la nyumbani kwa timu ya Singida United ambayo kwa sasa inatumia uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma katika michuano inayoendelea ya ligi licha ya makazi yake kuwa mkoani Singida.
Akizungumza Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba ambaye ndiye mdau mkubwa katika matengenezo hayo, amewahakikishia wapenzi wa kandanda mkoani humo kuwa uwanja huo utakuwa tayari kabla ya Novemba 4, 2017 na kuwataka wakazi wa Singida kujiandaa kuishangilia timu yao.
Kwa mujibu wa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Singida United imeweza kushika nafasi ya tatu kwa alama tisa ikiwa mbele kwa alama moja dhidi ya Yanga SC ambayo imeshika nafasi ya sita kwa pointi nane.

 Na eatv

Comments


Popular posts from this blog

DROO YA KLABU BINGWA ULAYA HII HAPA

Nyumba ya Mbunge Kigoma Mjini Zitto Kabwe yaungua moto

Cristiano Ronaldo kawaonesha watoto wake mapacha leo

Baada ya Kifo cha Mumewe… Zari Akwaa Aibu 5 #Tazama

hali ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu

Wapiga dili wa madini sasa kukiona

Irine Uwoya: afunguka kuhusu ombi la Dogo Janja kummiliki

hii ndio furaha ya Diamond na zari