CHADEMA yafunguka Hospitali aliolaza Tundu Lissu

Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeeleza kuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu aliyejeruhiwa kwa kupigwa risasi wiki iliyopita amelazwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya.
Chadema imetoa ufafanuzi huo baada ya taarifa za awali kueleza kuwa, Lissu anatibiwa katika Hospitali ya Aga Khan nchini humo.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Chadema, Tumaini Makene amesema leo Alhamisi kuwa, awali walipanga kumpeleka Hospitali ya Aga Khan lakini hilo lilibadilishwa baadaye.
Lissu alishambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi Septemba 7 akiwa nyumbani kwake Area D mjini Dodoma na siku hiyohiyo alisafirishwa kupelekwa Nairobi.
Kabla ya kusafirishwa saa sita usiku, Lissu ambaye pia ni mwanasheria wa Chadema na Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), alipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma.

  Na mwananchi

Comments


Popular posts from this blog

Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye ameitaka Serikali ya awamu ya tano kukivumilia

Mambo 10 ukiyazingatia wewe ni mke bora katika ndoa

Picha ya Beckham na mtoto wake Serengeti imeleta mjadala hadi kwao

Wasanii vinara kwa ushirikina watajwa

Emmanuel Mbasha, aweka wazi haya .

Tanzania inahifadhi wakimbizi wengi zaidi kutoka Burundi ukanda wa Afrika Mashariki

Aliyemuoa mwalimu wake ataka mahakama iwatenganishe bila sababu.

mimi nipo sex Lulu diva

Shamsa amuoneaa wivu Odama