SUGU;:Tundu lissu ameniagiza niwaambie haya

Joseph Mbilinyi amesema hayo baada ya kumtembelea Tundu Lissu jijini Nairobi nchini Kenya na kusema kutokana na uimara ambao Tundu Lissu anao amewataka Watanzania kujianda.
"Nimemtembelea 'Big hommie', Nairobi hospital. Ameniambia nikawaambie wana Mbeya kuwa alisikia mwitikio wao wa kishindo nilipomtaja kwenye jukwaa la muziki na kuwa mwili wake 'uliovunjwa vunjwa' kwa risasi unazidi kuimarika na atasimama tena. Ameniagiza niwaambie wana Mbeya na Watanzania wote wajiandae, wajiandae, wajiandae" alisema Sugu.
Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini,Mh. Joseph Mbilinyi pamoja na Mbunge wa Iringa Mjini juzi walimtembelea Tundu Lissu jijini Nairobi Kenya anapopatiwa matibabu kufuatia kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake mjini Dodoma Septemba 7, 2017.

Comments


Popular posts from this blog

Silole aweka wazi mambo

MBUNGE wa Nzega Mjini, Hussein Bashe ajitolea kwa wazee

, Mohammed Dewji nimechelewa

Zitto amjibu Spika, ahusisha mashtaka yake na Lissu

Diego Costa na Antonio Conte, ndani ya vita nzito