IGP Sirro atangaza bingo la milioni 10 Rufiji



Dar es Salaam. Mkuu mpya wa majeshi, IGP Simon Sirro amefanya mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari leo, na kutangaza dau nono la Sh10 milioni kwa atakayetoa taarifa kuhusu mauaji ya Kibiti, Rufiji na Mkuranga.
“Niwaambie ukweli kuwa katika hili, maneno yatakuwa machache lakini vitendo vitakuwa vingi zaidi,” amesema katika mkutano huo.
Pia IGP Sirro amewatangazia kiama madereva wa bodaboda na kuwataka kuacha kuvunja sheria za barabarani kwa makusudi.
“Huu ni wakati wa kutii utawala wa sheria bila shuruti na nimeshaongea na makamanda wa polisi nchi nzima,” amesema
BRIEFING
 Oktoba 2016
Kadhalika, Oktoba mwaka jana aliyekuwa Ofisa Mtendaji wa kijiji hicho Ally Milandu aliuawa baada ya kuvamiwa na watu wanne, waliompiga risasi mbili.
Novemba, 2016
Novemba mwaka jana, wenyeviti wawili wa vitongoji wa kijiji hicho waliuawa kwa kupigwa risasi.
Januari 2017
Januari mwaka huu, katika kijiji cha Nyambunda, kitongoji cha Mkwandara, watu wasiofahamika walimuua mfanyabiashara, Oswald Mrope kwa kumpiga risasi mbele ya familia yake.
Februari 2017
Tukio jingine ni lile la Februari 3, mwaka huu ambapo majambazi walivamia nyumba ya Mwenyekiti wa kijiji cha Jaribu, Bakari Msanga, ambaye alifanikiwa kuwatoroka.
Hata hivyo majambazi hayo yalipomkosa, yalirejea na kumwaga mafuta, kisha kuichoma moto nyumba yake.
 Februari 24
Februari 24 mwaka huu, majambazi hayo yalimuua ofisa upelelezi, wilaya hiyo, Peter Kubezya na maofisa maliasili wawili

Comments


Popular posts from this blog

Afariki kwakuchomwa na kisu

SUGU;:Tundu lissu ameniagiza niwaambie haya

VPL; Ngoma ngumu

STAR "ZARI THE BOSS LADY" APEWA USHAURI HUU

Messi amuandikia Neymar ujumbe huu.

Wabunge Uganda wataka kuondoa ukomo wa urais

Picha 10:madaraja makubwa na bora duniani

Jaji Mutungi ayatolea nje maamuzi ya CUF ya Maalim Seif

mimi nipo sex Lulu diva