IGP Sirro atuma salamu kwa wahalifu nchini

Mkuu wa Jeshi la Polisi, (IGP) Simon Sirro baada ya kuapishwa leo na Rais Magufuli amefunguka na kusema kazi yake ya kwanza kufanya ni kuhakikisha uhalifu unakwisha ili Watanzania waishi kwa amani nchini mwao.

    ais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mkuu wa Jeshi la Polisi, Kamishna wa Polisi Simon Sirro kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la polisi nchini Mei 29,2017 Ikulu jijini Dar es salaam

Simon Sirro amedai uhalifu nchini unaweza kupungua kama kutakuwa na ushirikiano mzuri kati ya wananchi na jeshi la polisi nchini sababu wahalifu hao wanaishi katika jamii zetu hizi hizi.

"Kipaumbele kikubwa ni uhalifu hivyo kazi yangu ni kuhakikisha uhalifu unapungua kwa kiasi kikubwa ili Watanzania waishi kwa amani lakini uhalifu huu utapungua tukipata ushirikiano mzuri na jamii, sababu hao wahalifu wanaishi kwenye jamii kwa hiyo ombi langu kwa Watanzania ili waishi kwa amani na utulivu ni vizuri sana watoe ushirikiano kwa jeshi la polisi. Naamini kabisa tutaweza sababu hawa wahalifu ni wachache kuliko sisi kwa hiyo umoja wetu ule lazima tutashinda" alisema Sirro

IGP Simon Sirro

Mbali na hilo IGP Sirro ametoa onyo kwa wahalifu wote nchini akiwataka waache mara moja kwani mwisho wa siku watapoteza tu maisha yao na kuacha familia zao zikipata shida.

"Lakini niwape onyo wahalifu kuwa uhalifu haulipi, kung'ang'ania uhalifu mwisho wa siku utaacha familia yako hivyo ni afadhali ufanye kazi ya halali itakusaidia kulea familia yako lakini ukijiingiza kwenye uhalifu wa ujanja ujanja haitakusaidia kitu, mwisho utaacha familia yako" alisisitiza IGP Sirro

Comments


Popular posts from this blog

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI 27.08.2017

Maajabu ya pacha walioungana, wajikuta katika penzi moja .

Picha sita 6 mende wamaajabu duniani

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 31.08.2017

TANZIA: Aliyewahi kuwa mbunge wa Moshi Mjini, Mzee Philemon Ndesamburo(CHADEMA) aaga dunia

Picha ya Beckham na mtoto wake Serengeti imeleta mjadala hadi kwao

MTWARA:watu watano wanashikiliwa na Jeshi la polisi

MANARA AMKABIDHI JPM KIWANDA

Jux afunguka haya kuhusu vanessa mdee

Marekani yatishia vikwazo kwa yeyote atakaekwamisha uchaguzi DRC