Wanasayansi nchini Marekani wamefanikiwa kupambana na maradhi sugu


Wanasayansi nchini Marekani wamefanikiwa kupambana na maradhi yaliyokuwa sugu kwa dawa za kupambana na vijidudu yaani antibiotics tatizo ambalo lilikuwa tishio dhidi ya sekta ya afya duniani.
Watafiti wameiboresha dawa ya sasa, Vancomycin kwa kutengeneza aina nyingine ya dawa.
Vancomycin ilikuwa ikipoteza uwezo wake wa kupambana na bacteria aitwae enterococci ambaye husabisha madhara kwenye njia ya haja ndogo na vidonda.
Aina mpya ya dawa hii ina nguvu mara elfu moja zaidi na hushambulia vijidudu kwa njia tatu tofauti, kiasi cha vijidudu kushindwa kupambana na dawa hiyo.
Inakadiriwa kuwa vijidudu vilivyokuwa vikipambana na dawa za antibiotics husababisha vifo takriban elfu hamsini kila mwaka nchini Marekani na barani Ulaya.

Comments


Popular posts from this blog

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI 27.08.2017

Maajabu ya pacha walioungana, wajikuta katika penzi moja .

Picha sita 6 mende wamaajabu duniani

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 31.08.2017

TANZIA: Aliyewahi kuwa mbunge wa Moshi Mjini, Mzee Philemon Ndesamburo(CHADEMA) aaga dunia

Picha ya Beckham na mtoto wake Serengeti imeleta mjadala hadi kwao

MTWARA:watu watano wanashikiliwa na Jeshi la polisi

MANARA AMKABIDHI JPM KIWANDA

Jux afunguka haya kuhusu vanessa mdee

Marekani yatishia vikwazo kwa yeyote atakaekwamisha uchaguzi DRC