waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mwigulu nchemba awajia juu Chenge, Werema

Wanasheria hao wakuu wa serikali wastaafu, ni Andrew Chenge na Jaji Frederick Werema na amewataka wamwache Rais John Magufuli aendelee kulinda rasilimali za umma, zisiliwe na watu wachache
         
Iramba.Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amewachana wanasheria wakuu wa Serikali wastaafu kwa kuwataka waeleze hadharani maslahi walionayo kwenye kampuni za madini zinazosafirisha mchanga nje ya nchi.
Wanasheria hao wakuu wa serikali wastaafu, ni Andrew Chenge na Jaji Frederick Werema na amewataka wamwache Rais John Magufuli aendelee kulinda rasilimali za umma, zisiliwe na watu wachache.
Mwingulu amesema hayo juzi wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na mamia ya wananchi wa Tarafa ya Ndago, jimbo la Iramba.
Alisema Chenge na Werema kwa nyakati tofauti wakiwa wanasheria wakuu wa Serikali, pamoja na majukumu yao mengine, wameshiriki kusaini mikataba mikubwa mikubwa, ikiwemo ya makampuni ya kuchimba madini.
“Kwa akili ya kawaida tu, baadhi ya mikataba mikubwa ikiwemo ya makampuni ya madini, haikuwa sawa… Ndio maana imelalamikiwa kwa muda mrefu,” alifafanua Mwigulu.

Comments


Popular posts from this blog

Mwezi Mtukufu… Roma Awafuturisha Watoto Yatima

Baada ya Kifo cha Mumewe… Zari Akwaa Aibu 5 #Tazama

Picha 10:madaraja makubwa na bora duniani

Wakili anayemtetea Mwanafunzi Abdul Nondo ameyasema haya

mimi nipo sex Lulu diva

Mchungaji Lusekelo ameandika ujumbe huo kwa jamii kuusu Tundulisu

Mara: Aua wawili nakujijeruhi