W.C.B MARUFUKU NIGHT CLUB



Kama wewe ni mtembeleaji mzuri wa kurasa za mitandao ya kijamii ya wasanii wa lebo ya WCB inayomilikiwa na Diamond Platinumz, bila shaka umekutana na uhaba mzito wa picha zinazowaonesha wakiwa klabu za usiku. Hii imetokana na marufuku inayowakabili!
Mpishi rasmi wa muziki wa WCB ndani ya Wasafi Records, mtarishaji Laizer amesema kuwa moja kati ya sera za lebo hiyo, zinakataza wasanii pamoja na mtayarishaji huyo kwenda kwenye klabu za usiku kula bata.
“Moja kati ya vitu ambavyo tunakatazwa ni kwenda klabu za usiku, hii hairuhusiwi kabisa,” Laizer aliiambia Twenzetu ya Times Fm. “Nadhani ni kwa sababu ya brand, haitakuwa kitu kizuri kuona brand inazurula tu usiku kwenye klabu na kama unavyojua klabu za usiku zina mambo mengi,” aliongeza.
Hata hivyo alisema kuwa wasanii hao wanaruhusiwa kuingia klabu kama kuna kazi au kuna mwaliko maalum utakaowasilishwa kwenye menejimenti kama mwaliko rasmi.
Endelea kubang tu na ngoma za WCB kwenye klabu ya usiku unayoikubali zaidi, lakini usitegemee kumuona Harmonize, Rich Mavoko, Raymond, Lava Lava hata bosi mwenyewe Chibu Dangote wakila bata karibu na wewe ndani ya klabu hizo bila mualiko maalum.

Comments


Popular posts from this blog

Afariki kwakuchomwa na kisu

SUGU;:Tundu lissu ameniagiza niwaambie haya

VPL; Ngoma ngumu

STAR "ZARI THE BOSS LADY" APEWA USHAURI HUU

Messi amuandikia Neymar ujumbe huu.

Wabunge Uganda wataka kuondoa ukomo wa urais

Picha 10:madaraja makubwa na bora duniani

Jaji Mutungi ayatolea nje maamuzi ya CUF ya Maalim Seif

mimi nipo sex Lulu diva