W.C.B MARUFUKU NIGHT CLUB



Kama wewe ni mtembeleaji mzuri wa kurasa za mitandao ya kijamii ya wasanii wa lebo ya WCB inayomilikiwa na Diamond Platinumz, bila shaka umekutana na uhaba mzito wa picha zinazowaonesha wakiwa klabu za usiku. Hii imetokana na marufuku inayowakabili!
Mpishi rasmi wa muziki wa WCB ndani ya Wasafi Records, mtarishaji Laizer amesema kuwa moja kati ya sera za lebo hiyo, zinakataza wasanii pamoja na mtayarishaji huyo kwenda kwenye klabu za usiku kula bata.
“Moja kati ya vitu ambavyo tunakatazwa ni kwenda klabu za usiku, hii hairuhusiwi kabisa,” Laizer aliiambia Twenzetu ya Times Fm. “Nadhani ni kwa sababu ya brand, haitakuwa kitu kizuri kuona brand inazurula tu usiku kwenye klabu na kama unavyojua klabu za usiku zina mambo mengi,” aliongeza.
Hata hivyo alisema kuwa wasanii hao wanaruhusiwa kuingia klabu kama kuna kazi au kuna mwaliko maalum utakaowasilishwa kwenye menejimenti kama mwaliko rasmi.
Endelea kubang tu na ngoma za WCB kwenye klabu ya usiku unayoikubali zaidi, lakini usitegemee kumuona Harmonize, Rich Mavoko, Raymond, Lava Lava hata bosi mwenyewe Chibu Dangote wakila bata karibu na wewe ndani ya klabu hizo bila mualiko maalum.

Comments


Popular posts from this blog

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI 27.08.2017

Maajabu ya pacha walioungana, wajikuta katika penzi moja .

Picha sita 6 mende wamaajabu duniani

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 31.08.2017

TANZIA: Aliyewahi kuwa mbunge wa Moshi Mjini, Mzee Philemon Ndesamburo(CHADEMA) aaga dunia

Picha ya Beckham na mtoto wake Serengeti imeleta mjadala hadi kwao

MTWARA:watu watano wanashikiliwa na Jeshi la polisi

MANARA AMKABIDHI JPM KIWANDA

Jux afunguka haya kuhusu vanessa mdee

Marekani yatishia vikwazo kwa yeyote atakaekwamisha uchaguzi DRC