STAR "SNURA" AWAASA WASANII CHIPUKUZI KUEPUKA KUTUMIA MADAWA YA KULEVYA.


Msanii wa muziki, Snura Mushi amewakanya vijana wanaotaka kuingia katika tasnia ya sanaa kuepuka vishawishi vya kujihusisha na matumizi ya dawa za kulevya huku akidai kufanya hivyo hakufanyi uonekane unaenda na wakati.
Snura amebainisha hayo baada ya kutuhumiwa akijihusisha na matumizi ya dawa za kulevya ambazo zinamfanya kumpa mizuka ya kufanya vizuri pindi akiwa stejini akitumbuiza.
“Vijana wenzangu kama mnaingia kwenye sanaa achaneni na vishawishi, kuna vishawishi vya kipumbavu sana, eti uonekane unaenda na wakati na ndiyo vinawaponza watu wanaingia kwenye dawa za kulevya huko wanavuta bangi eti mtu apate stimu afanye kazi vizuri nani kakwambia?,” Snura alikiambia kipindi cha Enez cha EATV.
“Mimi napanda kwenye steji situmii kilevi cha aina yeyote Mungu wangu aliyekuwa mbinguni ni shahidi sinywi pombe sivuti na nina panda kwenye steji nafanya vizuri tu kiasi kwamba wewe unaweza kufikiri nimetumia kilevi kwa sababu akili yangu nimeijenga kwamba hii ni kazi” aliongeza Snura.
Source:Bongo Newz

Comments


Popular posts from this blog

Uchumi wa taifa la Korea Kaskazini waimarika

harakati za ndesamburo na utajiri wake hizihapa

ACACIA wapinga vikali matokeo ya kamati ya pili ya Rais

IsraelIsrael yasalimu

mimi nipo sex Lulu diva

Real madrid mabingwa tena UEFA

Rais Zuma akiri kunusurika kuuawa kwa sumu

Hatua 10 Muhimi za Kumchagua Mchumba Mtakae Funga Ndo. a tzaama SOMA NA SHARE HII

Watu kumi na mmoja wauawa katika shambulio