Barnaba ammwagia sifa Dogo Aslay

Kupitia kipindi cha eNewz cha EATV Barnaba alisema anafurahishwa na jinsi nyimbo za Aslay zinavyopendwa na kupenya sana uswahilini bila msanii huyo kutumia nguvu kubwa ya kiki au 'interview' nyingi.
"Aslay yupo sawa kabisa, kitu kizuri ni kwamba mashabiki wanaongea wenyewe, uswahilini nyimbo zake zinapendwana sana na kwa sasa yeye ndiye msanii anayefanya vizuri kwa upande wangu" - Barnaba Classic
Aidha Barnaba alisema Aslay anaandika stori nzuri sana huku akiwakumbusha wasanii wakubwa kuangalia anachokifanya msanii huyo na kujifunza.
"Napenda sana anachokifanya Aslay, kwanza anaandika stori nzuri sana, mfano wimbo wake 'Mhudumu', au 'Danga' hata 'Ndoa" aliyomshirikisha Khadija Kopa" aliongeza msanii huyo.
Aslay alikuwa mmoja wa wasanii waliounda kundi la Yamoto Band ambapo kwa sasa anafanya kazi zake mwenyewe, tangu aanze kufanya kazi nje ya kundi Aslay ameshaachia nyimbo kama 'Angekuona', 'Usiitie Doa', 'Mhudumu', 'Baby' n.k

Comments


Popular posts from this blog

Mwezi Mtukufu… Roma Awafuturisha Watoto Yatima

Baada ya Kifo cha Mumewe… Zari Akwaa Aibu 5 #Tazama

Picha 10:madaraja makubwa na bora duniani

Wakili anayemtetea Mwanafunzi Abdul Nondo ameyasema haya

mimi nipo sex Lulu diva

Mchungaji Lusekelo ameandika ujumbe huo kwa jamii kuusu Tundulisu

Mara: Aua wawili nakujijeruhi