Barnaba ammwagia sifa Dogo Aslay

Kupitia kipindi cha eNewz cha EATV Barnaba alisema anafurahishwa na jinsi nyimbo za Aslay zinavyopendwa na kupenya sana uswahilini bila msanii huyo kutumia nguvu kubwa ya kiki au 'interview' nyingi.
"Aslay yupo sawa kabisa, kitu kizuri ni kwamba mashabiki wanaongea wenyewe, uswahilini nyimbo zake zinapendwana sana na kwa sasa yeye ndiye msanii anayefanya vizuri kwa upande wangu" - Barnaba Classic
Aidha Barnaba alisema Aslay anaandika stori nzuri sana huku akiwakumbusha wasanii wakubwa kuangalia anachokifanya msanii huyo na kujifunza.
"Napenda sana anachokifanya Aslay, kwanza anaandika stori nzuri sana, mfano wimbo wake 'Mhudumu', au 'Danga' hata 'Ndoa" aliyomshirikisha Khadija Kopa" aliongeza msanii huyo.
Aslay alikuwa mmoja wa wasanii waliounda kundi la Yamoto Band ambapo kwa sasa anafanya kazi zake mwenyewe, tangu aanze kufanya kazi nje ya kundi Aslay ameshaachia nyimbo kama 'Angekuona', 'Usiitie Doa', 'Mhudumu', 'Baby' n.k

Comments


Popular posts from this blog

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI 27.08.2017

Maajabu ya pacha walioungana, wajikuta katika penzi moja .

Picha sita 6 mende wamaajabu duniani

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 31.08.2017

TANZIA: Aliyewahi kuwa mbunge wa Moshi Mjini, Mzee Philemon Ndesamburo(CHADEMA) aaga dunia

Picha ya Beckham na mtoto wake Serengeti imeleta mjadala hadi kwao

MTWARA:watu watano wanashikiliwa na Jeshi la polisi

MANARA AMKABIDHI JPM KIWANDA

Jux afunguka haya kuhusu vanessa mdee

Marekani yatishia vikwazo kwa yeyote atakaekwamisha uchaguzi DRC