Siku kadhaa zilizopita Rais wa Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF), Jamal Malinzi alitoa taarifa kupitia ukurasa wake wa Twitter akielezea juu ya barua iliyokuwa ikihusu ubingwa wa Yanga, sasa habari kamili TFF wameitoa nayo ni hii hapa: Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa (FIFA), Gianni Infantino, Mei 24, mwaka huu alituma ujumbe Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuipongeza Young Africans ya Dar es Salaam kwa kutwaa ubingwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2016/17. Young Africans imetwaa Kombe hilo ikiwa ni mara tatu mfululizo na katika salamu za pongezi, Rais Gianni Infantino amesema ubingwa huo wa Young Africans ni kielelezo cha ushirikiano baina ya wachezaji, kocha, utawala, matabibu pamoja na mashabiki. Katika pongezi zake Rais Infantino ameishukuru Young Africans na shirikisho la mpira wa miguu la nchi kwa kusadia kupeleka ujumbe chanya kwa jamii kuhusiana na mpira wa miguu. TANGAZA NASI HAPA
Ni asubuhi nyingine tena nakukutanisha na habari kubwa kwenye Magazeti ya Tanzania leo September 30 2017 kua nzia ya Udaku, Michezo na Hardnews kujionea yote makubwa yaliyoandikwa
Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga SC, Charles Boniface Mkwasa amemtangaza rasmi mshambuliaji, Ibrahim Ajib Migomba kujiunga na timu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili. “Tuna mtambulisha rasmi kwa wapenzi wa Yanga na wanamichezo kwa ujumla mchezaji, Ibrahim Ajib ambaye kwa hivi sasa amepata kandarasi ya miaka miwili kuichezea klabu ya Yanga”. “Tumekuwa tukisikia kwenye vyombo vya habari na tumekuwa tukisema tutaendelea kutangaza wachezaji kwa wakati maalumu kama ilivyokuwa leo tumeamua kumtangaza rasmi Ajibu na natumia fursa hii kumpokea” amesema Charles Boniface Mkwasa katibu Mkuu wa klabu ya Yanga. Uwezo wake mkubwa wa kumiliki mpira na kufunga ndio sababu ya wadau wengi kuamini mshambuliaji huyu wa Yanga anaweza kuwa mmoja wa watakao weza kuisadia klabu hiyo katika mashindano ya kitaifa na kimataifa ambayo wanakabiliwa nayo.
MSANII WA MAIGIZO ALIYEFANYA VIZURI NA FILAMU YA 'MAPENZI YA MUNGU', ELIZABETH MICHAEL ' LULU' AMEFUNGUKA NA KUSEMA WASANII WA MAIGIZO BONGO WANAFELI KUTOKANA NA KUTOJIELEWA NI KITU GANI AMBACHO WANAKITAKA KWENYE SANAA, BADALA YAKE WANAFUATA MIKUMBO. LULU AMEFUNGUKA HAYO HIVI KARIBUNI AKIZUNGUMZA NA WANAHABARI NA KUSEMA KUWA WASANII WENGI WA TANZANIA HAWAPENDI KUJISHUGHULISHA KUTAFUTA KITU KIZURI KWA KUWA WENGI WAO WALIFUATA MKUMBO KWENYE KUIGIZA NA WENGINE WALICHUKULIA KAMA SEHEMU YA KUJIPATIA UMAARUFU ILI MAISHA YAENDELEE AU SEHEMU YA KUPOTEZEA MUDA. "UKWELI UPO KWENYE UIGIZAJI KUNA WATU TUNACHUKULIA HII NI KAZI, WAPO WANAOFANYA KAMA SEHEMU YA KIPAJI CHAKE LAKINI PIA WAPO AMBAO WANACHUKULIA KAMA SEHEMU YA KUJIPATIA UMAARUFU AU KU-REFRESH KWANI WANAKUA NA KAZI ZAO ZINGINE, NA HAO NDIO WANAOSABABISHA TUONEKANE WAIGIZAJI WA MUVI TUMEFELI". PAMOJA NA HAYO LULU AMEONGEZA, "UNAJUA PIA KUFUATA MKUMBO NI KITU KILICHOTURUDISHA NYUMA. WATU WENGI WALIKUWA W...
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bw. Waziri Waziri Kindamba kuwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL). Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa Uteuzi wa Bw.Waziri Waziri Kindamba umeanza tarehe 04 Julai, 2017. Kabla ya uteuzi huo, Bw. Waziri Waziri Kindamba alikuwa akikaimu nafasi hiyo
Jeshi la polisi lilikwenda nyumbani kwa Tundu Lissu kufanya ukaguzi kufuatia makosa mawili ambayo Mbunge huyo wa Singida Mashariki na Rais wa TLS anatuhumiwa nayo ambayo ni pamoja na Kusema makosa ya Rais John Pombe Magufuli hadharani na chochezi kuhusu kushikiliwa ndege ya Tanzania aina ya Bombardier Q400 huko nchini Canada. Kwa mujibu wa Afisa Habari wa CHADEMA, Tumaini Makene amedai kuwa Tundu Lissu amerudishwa Kituo Kikuu cha Polisi kwa ajili ya taratibu zingine za kisheria ambazo zitaendelea ikiwa pamoja na dhamani ambayo kisheria ipo wazi. Tundu Lissu alikamatwa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2017 na jeshi la polisi alipotoka mahakamani kwenye kesi ya uchochezi , alipelekwa Police Central kwa ajili ya kufanyiwa mahijiano na baadaye kulala rumande kutokana na jana kushindwa kupewa dhamana. Na eatv
Comments