Mwanafunzi wa shule ya sekondari Nzasa amefariki dunia baada ya kuchomwa kisu shingoni kwa kisa kinachodaiwa kugombea mwanamke. Mwanafunzi huyo Ashiri Musa ambae alikua anasoma kidato cha nne shule ya sekondari Nzasa alikutwa na tukio hilo jana majira ya usiku ambapo alichoma kisu shingoni na kupekea kuvuja damu nyingi ambazo zilipelekea kifo chake papohapo. Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa Temeke alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema mtuhumiwa wa tukio hilo anashikiliwa na jeshi la polisi kwa uchunguzi zaidi. Na JF
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe amewashukuru wavamizi wa Msitu wa Hifadhi wa Isawima wilayani Kaliua ambao wameamua kwa hiari yao kubomoa makazi na kuondoka wao na mifugo yao katika eneo hilo ambalo ni miongoni mwa vyanzo vya maji ya Ziwa Tanganyika . Ameyasema hayo Wilayani Kaliua mara baada ya kusomewa taarifa ya utekelezaji wa zoezi la kuwaondoa Wavamizi hao katika Msitu wa Hifadhi na kutembelea eneo walipoondolewa wavamizi na kisha kupata fursa ya kuongea na wananchi. Amesema kuwa Serikali imefurahishwa na uamuzi huo uliochukuliwa na watu hao baada ya kupata elimu kuhusu athari za kimazingira za wao kung’ang’ania kuendelea kuishi katika maeneo yaliyohifadhiwa na kuamua kuondoka bila kushurutishwa. “Serikali haina shida ya kumuonea mtu na ndio maana tumekuwa tukiitumia zaidi elimu jambo ambalo limeleta mafaniko makubwa katika eneo la Hifadhi hii ambapo zaidi ya asilimia ya 70 ya watu waliokuwa wamevamia wameondoka,”amesema Prof. Maghembe
Katibu wa Halmashauri Kuu Itikadi na Uenezi (CCM) Humphrey PolePole amesema kuwa mchakato wa kuwashughulikia viongozi mbalimbali ambao wanatuhuma mbalimbali umeanza na kusema wao watatenda haki kwa kuwapa nafasi ya kujieleza juu ya shtuma hizo au kashfa hizo na baadaye uongozi wa chama utafanya maamuzi juu ya watu hao. " Serikali hii imejikita kutetea na kusimamia haki na kuhakikisha uadilifu unasimamiwa na hakika haki itasimamiwa na mchakato mzuri wetu wa chama kuhakikisha kwamba mtu ameulizwa, amepewa tuhuma zake na amejitetea lakini sisi tunafanya uamuzi na tumeshakwisha anza kufanya uamuzi toka mwaka jana na mwaka huu katika vikao vinavyokuja na hakika Watanzania wawe na masikio tayari kuweza kujua na tutaendelea kudhihirishia Umma kuwa tunamaanisha kwenye mambo ya maadili" alisema Polepole Rais Magufuli aliwahi kumuomba Spika wa Bunge, Job Ndugai kuwa Bungeni wanaweza kuwa utaratibu wao kuwaandikia viongozi wa vyama vya siasa juu ya wabunge mbalimbali ambao wanakuwa...
Mwandishi wa Mwananchi Tumaini Msowoya na Mkuu wa Kituo cha Nyota ya Asubuhi, Sister Idda Luizer wakiwa na mapacha, Maria na Consolata By Tumaini Msowoya, Mwananchi tmsowoya@mwananchi.co.tz Jana tuliishia sehemu inayoeleza jinsi pacha hawa walioungana, Maria na Consolata, wanavyochangia hisia za baadhi ya viungo vyao. Pengine ni kuchangia huko kwa hisia za viungo, kumefanya wawe pia na hisia moja katika masuala ya kimaisha. Wawili hawa wanahisia moja ya kimapenzi. Sasa endelea… Si rahisi kufikiria maisha ya ndoa ya Maria na Consolata kwa jinsi walivyo, lakini pacha hawa walioungana wako wazi kuhusu matamanio yao ya maisha ya ndoa. Katika mazungumzo yao na gazeti hili, Maria na Consolata waliweka bayana mipango yao ya ndoa mara watakapomaliza elimu ya chuo kikuu. Ingawa ni kitu cha kushangaza, Maria na Consolata hawatakuwa mapacha wa kwanza katika maisha ya ndoa. Chang na Eng Bunker ni pacha wanaume waliozaliwa mwaka 1811 nchini Thailand ambako zamani kuliitwa Siame. ...
Benjamin Fernandes ni Mtanzania ambaye ameingia kwenye headlines katika mitandao mbalimbali baada ya kuhitimu Masters kwenye Chuo Kikuu cha Biashara kinachotajwa kuwa Namba moja Duniani, Stanford, Marekani. Benjamin anayo hii story nyingine baada ya kukataa ofa za kufanya kazi kwenye makampuni makubwa ambayo yalikuwa tayari kumlipa hadi Tsh. 425m kwa mwaka kama angekubali kufanya kazi akiwa Marekani. >>Watu wengi wananiuliza kwa nini nimerudi? Kwa nini nimerudi nyumbani? Kweli nilikuwa napewa ofa za Shilingi 425m kwa mwaka kufanya kazi Marekani kwenye kampuni mbalimbali. Mpaka leo asubuhi nimepigiwa simu na kampuni kutoka Marekani ni kampuni kubwa sana.” Na Millard ayo.com
Ni siku 21 baada ya staa wa kimataifa wa Brazil aliyekuwa anaichezea FC Barcelona Neymar aamue kuihama club hiyo na kujiunga na Paris Saint Germain ya Ufaransa kwa rekodi ya dunia ya pound milioni 199, leo FC Barcelona wamesajili mbadala wake. FC Barcelona ambao walikuwa wamelenga kumsajili mbrazil Philippe Coutinho kutoka Liverpool au Ousmane Dembélé kama chaguo lao la pili kama wakimkosa Coutinho , leo August 25 wamefanikiwa kumsajili Ousmane Dembélé kwa uhamisho wa pound milioni 96 ambazo zinaweza kuongezeka hadi kufikia pound milioni 136. Kwa uhamisho huo sasa Ousmane Dembélé mwenye umri wa miaka 20 ndio anakuwa mchezaji wa pili ghali zaidi duniani baada ya Neymar , Dembele amesajiliwa akitokea Borussia Dortmund ya Ujerumani, maamuzi hayo ya FC Barcelona yamekuja baada ya kuka...
Msanii wa Bongo Fleva, Timbulo amedai yeye anampenda mwanamke yeyote ila kuna wakati unafika anachanganyikiwa katika kuchagua. Muimbaji huyo ameeleza kuchanganyikiwa huko kunakuja pale anapompenda wanamke mweusi lakini anapomuona mwanamke mweupe anakuwa anavutiwa nae zaidi. “Nikawa najiuliza hii inakuaje haya nasema napenda mwanamke vimodo lakini nikiona mwanamke mwenye umbo kubwa nachanganyikiwa, baadaye nikaja kugundua mimi mjinga moyo wangu unanidanganya, kumbe natakiwa kupenda kile ambacho kitakuwepo kwa wakati uliopo,” amesema Timbulo. Ameongeza, “Kwa hiyo mimi sijawahi kuwa na ‘choice’ kwamba napenda mwanamke wa hivi au hivi inategema na wakati tu siku zingine napenda mweusi, mweupe, mwembamba au unene” amesisitizaTimbulo
Polisi nchini Uhispania imewaokoa wanawake 13 waliokuwa wakifanya kazi ya ukahaba na uporaji watu katika mji wa Puerto Banus. Wanawake hao ambao kwa sasa wapo huru waliletwa katika eneo hilo, wakitokea nchini Bulgaria, na walifika hapo wakalazimishwa kufanya kazi za ukahaba katika kituo kimoja cha utalii. Inaelezwa kuwa wanawake hao walilazimishwa pia kufanya biashara ya uporaji mali mtaani na kutumia madawa ya kulevya. Kukamatwa kwa watu hao, kumekuja takribani miaka mitatu baada ya polisi kujulishwa kuhusu mtandao huo. Polisi wamefanikiwa kuwatia mbaroni watuhumiwa 34 ambao walikuwa wakihusika na mtando huo katika nchi zote mbili, pia wamekamata mali zao kama vile magari na kuzifungia akaunti zao za kibenki ilikufanya uchunguzi.
Katika majadiliano hayo Rais Uhuru amesema yuko tayari kwa uchaguzi na hana matakwa yoyote kutoka IEBC, zaidi ya chombo hicho kutekeleza wajibu wake wa kusimamia uchaguzi mpya wa raia Oktoba 26 kama ulivyoamriwa na Mahakama ya Juu. Kikao hicho kilifanyika katika Jengo la Harambee, ambako imo ofisi ya Rais katikati ya jiji na kilihudhuriwa pia na Makamu wa Rais William Ruto. “Tuliweka wazi kwamba hatuna matakwa au masharti kuhusu suala hili. Tumetenga fedha kwa ajili ya IEBC kufanya kazi yake. Sasa watekeleze wajibu wao,” alisema Rais. “Tunasisitiza kwamba uchaguzi ufanyike Oktoba 26, muda uliopangwa na IEBC kama masharti baada ya uchaguzi wa Agosti 8 kufutwa,” aliongeza. Septemba Mosi, Mahakama ya Juu ilifuta matokeo ya urais ya Agosti 8 ikidai ilijiridhisha kwamba ulijaa dosari na kukosa uhalali. Tangu wakati huo Rais na makamu wake wamefanya kampeni nzito katika kaunti zote kwa ajili ya uchaguzi huo wa marudio.
Mkali wa muziki wa Hip Hop Bongo, Ibrahimu Musa ‘Roma Mkatoriki, baada ya juzi kuibukia Shule ya Mchikichini iliyopo Mbagala Rangi Tatu, jana Ijumaa Juni 16 mkali huyo alifuturu na watoto yatima katika kituo cha Dira kilichopo mitaa ya kwa Mzungu Mbagala Jijini Dar. Akizungumza na Global TV Online, Roma alisema aumuzi wa kwenda kufuturu na watoto yatima katika kituo hicho umekuja baada ya kuona ana kila sababu ya Kuungana na watoto yatima na kuwatia moyo katika maisha yao kuelekea kilele ya siku ya watoto duniani. “Tuko katika maadhimisho ya siku ya watoto ulimwenguni, kimisingi nimefurahi kufuturu pamoja na watoto yatima wa kituo hiki. “Lakini pia nimepata nafasi ya kuwatia moyo na kuzungumza nao mambo mbalimbli kuhusu maisha, watoto pia wamefurahi kuniona na wamepata fursa ya kuniuliza mambo mengi. “Nimeambiwa kuna changamoto nyingi hapa kituoni, nimewahidi nitafanya kila liwezekanalo kuhakikisha changamoto zile tunazimaliza siku za hivi karibuni kwa kushirikiana na wasani...
Comments