Liverpool watapambana na Hoffenheim ya Ujerumani ili kufuzu kucheza ngazi ya makundi ya UEFA Klabu Bingwa Ulaya. Liverpool watacheza ugenini duru ya kwanza Agosti 15 au 16, na marudiano Anfield Agosti 22 au 23. Washindi 10 katika mechi hizo za kufuzu wataungana na timu 22 ambazo tayari zimefuzu kucheza ngazi ya makundi ya Uefa Champions League. Mechi nyingine ni kama ifuatavyo: Sporting Lisbon (Portugal) v Steaua Bucharest (Romania) Hoffenheim (Germany) v LIVERPOOL (England) Napoli (Italy) v Nice (France) Young Boys (Switzerland) v CSKA Moscow (Russia) Istanbul Basaksehir (Turkey) v Sevilla (Spain) Hapoel Beer-Sheva (Israel) v NK Maribor (Slovenia) CELTIC (Scotland) v Astana (Kazakhstan) Olympiacos (Greece) v NK Rijeka (Croatia) APOEL Nicosia (Cyprus) v Slavia Prague (Czech Republic) Qarabag FK (Azerbaijan) v Copenhagen (Denmark)
Nyumba ya Mbunge Kigoma Mjini Zitto Kabwe aliyoijenga wakati akigombea ubunge kwa mara ya kwanza iliyopo Kibingo, Kata ya Mwandiga mjini Kigoma imeungua moto jioni hii. Nyumba hiyo iko kiwanja kimoja na nyumba yake ya sasa imeteketea yote na chanzo chake hakijafahamika hadi sasa. Msaidizi wa mbunge huyo, Nyembo Mustafa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba hata hivyo Zitto hakuwa anaishi kwenye nyumba hiyo. Amesema Zitto alihama kwenye nyumba hiyo baada ya kujenga nyumba nyingine kubwa kwenye kiwanja hicho hicho na iliyoungua ilikuwa ikitumika kwa dharura.
Zikiwa zimepita siku kadhaa toka staa wa soka wa kimataifa wa Ureno anayaeichezea Real Madrid ya Hispania Cristiano Ronaldo atangaze kuwa amepata watoto mapacha wawili, leo June 29 amepost picha akiwa na mapacha hao. Ronaldo ambaye timu yake ya taifa ya Ureno ambayo yeye ni nahodha wametolewa jana kwa mikwaju ya penati dhidi ya Chile, leo kuwaonesha hadharani watoto wake mapacha kwa kupost picha kwa mara ya kwanza.
KAMPALA: Katikati ya majonzi, yapata siku 15 tu tangu mumewe, Ivan Ssemwaga ‘Ivan Don’ azikwe huko Nakalilo nchini Uganda baada ya kufariki dunia ghafla, aliyekuwa mkewe, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, anadaiwa kuwatibua Waganda kufuatia kushiriki matukio matano (5) yanayotafsiriwa kuwa ni ya aibu, Amani linayo. Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya udaku nchini Uganda, tofauti na ilivyotarajiwa, kama ilivyo kwa baadhi ya tamaduni za Kiafrika, kuwa Zari angekuwa kwenye maombolezo kwa siku arobaini au hadi amalize eda kwa kufi wa na mume huyo, yeye amekuwa akijihusisha na ishu ambazo zinaacha watu midomo wazi. AIBU YA KWANZA Ilielezwa kwamba, siku mbili tu baada ya mazishi ya Ivan, Mei 30, mwaka huu, Zari alitupia video kwenye akaunti yake ya Mtandao wa Kijamii wa Snapchat ikimuonesha mwenye furaha tele huku akikata mauno ya hatari hivyo kushangaza wengi walioamini ni video ya zamani. Ilisemekana kuwa, ili kuonesha video hiyo haikuwa ya zamani, Zari aliambatanisha na maneno ya
Ni asubuhi nyingine tena nakukutanisha na habari kubwa kwenye Magazeti ya Tanzania leo August 21 2017 kuanzia ya Dini, Michezo na Hardnews kujionea yote makubwa yaliyoandikwa.
Mchungaji Peter Msigwa amesema hali ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu inaendelea vizuri na anatamani apate nafuu na kunyoosha vidole viwili (ishara ambayo hutumiwa na Chadema). Akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalum leo Jumatano jioni jijini Dar es Salaam, Mchungaji Msigwa amesema kwa kipindi chote hicho Lissu hakuwa akila na hali yake imebadilika ukilinganisha na alivyokuwa hapo awali lakini hivi sasa anakula vitu laini. kabla sijaanza safari ya kuja (kurudi Dar es Salaam) amenitania sana kwa kusema anatamani apate nafuu na kuonyesha alama ya vidole viwili,” amesema Mchungaji Msigwa. Msigwa ameeleza wanaendelea kujadiliana na madaktari ili kuangalia uwezekano wa kumpeleka nchi nyingine kwa ajili ya matibabu zaidi. Amesema Lissu anaangaliwa na madaktari 10 kila mmoja akishughulika na eneo lake ili kuhakikisha hali yake inatengemaa. “Miongoni mwa mambo anayoyarudia ni kututaka kuendelea kupambana, kupaza sauti kuikomboa nchi, ”amesema Msigwa.
Baada ya kutolewa kwa ripoti ya kamati mbili za bunge kuhusu biashara ya madini ya almasi na Tanzanite, vigogo wote waliohusika katika kuisababishia hasara serikali wanakabiliwa na hatari ya kufilisiwa mali zote wanazomiliki. Hali hiyo imejidhihirisha mara baada ya Serikali kumtaka Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Mganga Bisawalo kuhakikisha ushahidi unapatikana na wahusika wanafikishwa mbele ya mkono wa sheria. Aidha, agizo hilo limetolewa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango wakati wa kukabidhiwa kwa mzigo wa madini ya almasi uliokamatwa Septemba Mosi mwaka huu Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (JNIA). “Hali ya taifa kuendelea kuibiwa haivumiliki hata kidogo katika kipindi hiki ambacho Serikali ingali inapambana kuhakikisha kuwa watanzania wananufaika na rasilimali zao, DPP hakikisha ushahidi unapatikana haraka zaidi ili sheria ichukue mkondo wake,”amesema Dkt. Mpango
Wiki kadhaa baada ya Dogo Janja aka Janjaro kuweka wazi kwenye vyombo vya habari kuwa muigizaji Irine Uwoya ndiye anayemkosesha usingizi na angependa siku moja awe barafu wa moyo wake, Uwoya amemfungukia. Janjaro aliwahi kusema kuwa, “Irene Uwoya nampenda tangu nikiwa mtoto, nimeshabandika sana picha yake maghetoni. Nampendaga sana na ni mtu ambaye nammezeaga mate.” Muigizaji huyo ambaye amekuwa akitajwa mara kwa mara kwenye nyimbo za wasanii wa Bongo Flava akihusishwa na mfano wa uzuri na mvuto, amekejeli ombi la Janjaro ambaye amedai ni mdogo wake mwenye matatizo yake binafsi. “Yaani kale jamani… ni mdogo wangu, naongeaga naye tunapiga story. Kananifurahisha lakini, hivyo tu,” Uwoya aliiambia Dizzimonline. Hata hivyo, Uwoya aliweka wazi kuwa katika kumchagua mwandani yake, umri sio kigezo cha kumpima mwanaume anayetaka kuwa naye.
Kupitia mtandao wa instagram, wazazi hao wameshindwa kuzuia furaha zao juu ya mtoto wao huyo. Diamond ndio amekuwa wa kwanza kuandika ujumbe wake kwenye mtandao huo, “Happy 2 years mama, Words Can’t express how much i love you my Tee…. @princess_tiffah Naye Zari hakusita kuonyesha furaha yake kwa kuandika, “It’s princess world…happy birthday my one and only @princess_tiffah.” “My Princess….. May God see you through with nothing but the best. May you be blessed from this day forward. Most of all, May you be a Godly child. Without God we are nothing. Happy birthday @princess_tiffah,” amesndika kwenye picha nyingine ya mtot wao huyo aliyoiweka kwenye mtandao huo
Comments