Mkali wa muziki wa Hip Hop Bongo, Ibrahimu Musa ‘Roma Mkatoriki, baada ya juzi kuibukia Shule ya Mchikichini iliyopo Mbagala Rangi Tatu, jana Ijumaa Juni 16 mkali huyo alifuturu na watoto yatima katika kituo cha Dira kilichopo mitaa ya kwa Mzungu Mbagala Jijini Dar. Akizungumza na Global TV Online, Roma alisema aumuzi wa kwenda kufuturu na watoto yatima katika kituo hicho umekuja baada ya kuona ana kila sababu ya Kuungana na watoto yatima na kuwatia moyo katika maisha yao kuelekea kilele ya siku ya watoto duniani. “Tuko katika maadhimisho ya siku ya watoto ulimwenguni, kimisingi nimefurahi kufuturu pamoja na watoto yatima wa kituo hiki. “Lakini pia nimepata nafasi ya kuwatia moyo na kuzungumza nao mambo mbalimbli kuhusu maisha, watoto pia wamefurahi kuniona na wamepata fursa ya kuniuliza mambo mengi. “Nimeambiwa kuna changamoto nyingi hapa kituoni, nimewahidi nitafanya kila liwezekanalo kuhakikisha changamoto zile tunazimaliza siku za hivi karibuni kwa kushirikiana na wasani...
KAMPALA: Katikati ya majonzi, yapata siku 15 tu tangu mumewe, Ivan Ssemwaga ‘Ivan Don’ azikwe huko Nakalilo nchini Uganda baada ya kufariki dunia ghafla, aliyekuwa mkewe, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, anadaiwa kuwatibua Waganda kufuatia kushiriki matukio matano (5) yanayotafsiriwa kuwa ni ya aibu, Amani linayo. Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya udaku nchini Uganda, tofauti na ilivyotarajiwa, kama ilivyo kwa baadhi ya tamaduni za Kiafrika, kuwa Zari angekuwa kwenye maombolezo kwa siku arobaini au hadi amalize eda kwa kufi wa na mume huyo, yeye amekuwa akijihusisha na ishu ambazo zinaacha watu midomo wazi. AIBU YA KWANZA Ilielezwa kwamba, siku mbili tu baada ya mazishi ya Ivan, Mei 30, mwaka huu, Zari alitupia video kwenye akaunti yake ya Mtandao wa Kijamii wa Snapchat ikimuonesha mwenye furaha tele huku akikata mauno ya hatari hivyo kushangaza wengi walioamini ni video ya zamani. Ilisemekana kuwa, ili kuonesha video hiyo haikuwa ya zamani, Zari aliambatanisha na maneno ya...
Zifuatazo ni Picha za Madaraja [Bridges] yenye Ubora na Ukubwa hapa Duniani na yanapopatikanapo; 1. Danyang-Kunshan Grand Bridge(Daraja) Hili ni Daraja lenye urefu zaidi ya Kilometre 164 ;Linapatikana CHINA. 2.Tianjin Grand Bridge Urefu ni zaidi ya Kilometre 100 ; Mahali ni CHINA 3.Weinan Weihe Grand Bridge Urefu wa Daraja hilo ni Kilometre 79.7 ; Mahali CHINA 4.Bang Na Expressway Urefu wa Daraja hilo ni Kilometre 56 , Mahali THAILAND 5.Beijing Grand Bridge(Beautiful Bridge) Urefu wa Daraja hilo ni Kilometre 48 ; Mahali CHINA 6.Lake Pontchartrain Causeway Urefu wa Daraja hilo ni Kilometre 38.35 ; mahali U.S.A [MAREKANI] 7 .Manchac Swamp Bridge Urefu wa jumla ni Kilometre 36.69 ; Mahali U.S.A [MAREKANI] 8.YangCun Bridge Urefu wa Daraja hilo ni Kilometre 35.8 ; Mahali ni CHINA 9.Hangzhou Bay Brigde Ure...
Wakili anayemtetea Mwanafunzi Abdul Nondo, ambaye Jeshi la Polisi linamshikilia kwa upelelezi kufuatia madai ya kutekwa, amesema mpaka sasa yeye na wenzake wamefanya kila jitihada za kumuona mteja wao pasipo mafanikio. "Kwa jitihada nilizofanya mpk sasa kumuona Abdul Nondo hazijazaa matunda. Hayupo vituo vikuu vyote, tukutane HC kupitia Habeus Corpus watamleta wenyewe!" amesema Wakili Jebra Kambone. Kauli hii ameitoa kufuatia Kamanda Mambosasa kusema taarifa za Wakili huyo kuwa amezuiwa kumuona kijana huyo ni za uongo.
Muimbaji Lulu amekiambia kipindi cha Uhondo cha E Fm kuwa alitambua kuwa yeye ni mzuri kutokana na sifa alizokuwa akipewa na mama yake mzazi kitu ambacho kilimfanya kutolaghaika na watu waliokuwa wakimsifia. “Mimi ni msichana ambaye nipo sex ambaye nina mvuto, mama yangu alikuwa akiniambia Lulu mwanangu mashallah, yaani hapa sidhani kama kuna mtu nitamwambia idadi ya ng’ombe ninazozitaka halafu akapindua,” amesema na kuongeza. “Na mimi mwenyewe nikawa najiona ndio maana hata sikuweza kurubunika, yaani ile mtu kuniambia wewe mzuri akanidanganya kwa vichipsi mayai, mwenyewe nilishajijua ni mzuri,” amesema Lulu Diva. Hitmaker huyo wa Usimwache kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake inayokwenda kwa jina la Utamu.
Mchungaji Lusekelo ameandika ujumbe huo kupitia kwenye mitandao yake ya kijamii na kusema kuwa mbona watu hao hawakuonekana kulaani mauaji ya Kibiti au kuitisha maombezi baada ya watu Kibiti kuuawa. "Tusitumie tatizo la ndugu yetu Tundu lissu kujipatia umaarufu wa kisiasa au wakidini, mtu yeyote ambaye anatumia tukio hili kujipatia umaarufu wa kisiasa au wakidini namfananisha na wale wahuni ambao basi likianguka anaenda kuchukua simu kwanza, ni jambo ovu sana wewe unakuwa ni sehemu ya watu walio mpiga risasi Tundu lissu. Mwenzako anaumwa wewe unatumia ugonjwa wake kujipatia umaarufu wa kidini au wakisiasa ni jambo baya sana, mbona sikusikia wakilaani mauaji ya kibiti au kuitisha maombezi watu wakibiti walipo uwawa, mbona hawaja laani utekaji na mauaji ya watoto Arusha hata wa Marekani (umoja wa ulaya) sikusikia wanalaani mauaji ya kibiti" aliandika Mzee wa Upako Aidha Mchungaji huyo amesema kuwa yeye anaamini watu hao wanatumia matatizo ya Tundu Lissu kujiongezea umaaru...
Watu wawili wamefariki dunia na mwingine mmoja kujijeruhi baada ya kutokea ugomvi unaohusishwa na wivu wa mapenzi mjni Bunda. Tukio hilo lilitokea jana saa tano asubuhi katika Mtaa wa Bunda Stoo baada ya mtu mmoja kuwavamia watu wawili kisha kuwachoma visu kabla ya kujichoma mwenyewe. Akizungumza mjini hapa, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, Jaffari Mohamed alisema jana kuwa waliouawa ni Daudi Phares (29) mkazi wa Bunda na msichana aliyetambulika kwa jina moja la Monica (22) mkazi wa Magu mkoani Mwanza. Kamanda huyo alimtaja aliyejijeruhi baada ya kujichoma kisu maeneo mbalimbali mwilini mwake kuwa ni Selemani Jeremia (33) ambaye ni mkazi wa Magu. Alisema kuwa siku ya tukio Selemani alisafiri kutoka Magu mkoani Mwanza hadi Bunda ambapo alifika nyumbani kwa Daudi na kumkuta akiwa na Monica. Baada ya kufika nyumbani hapo Selemani alianza kumchoma visu Dauidi katika sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwamo kifuani upande wa kushoto na kusababisha kifo chake papo hapo. Alisema kuw...
Comments