Mwanafunzi wa shule ya sekondari Nzasa amefariki dunia baada ya kuchomwa kisu shingoni kwa kisa kinachodaiwa kugombea mwanamke. Mwanafunzi huyo Ashiri Musa ambae alikua anasoma kidato cha nne shule ya sekondari Nzasa alikutwa na tukio hilo jana majira ya usiku ambapo alichoma kisu shingoni na kupekea kuvuja damu nyingi ambazo zilipelekea kifo chake papohapo. Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa Temeke alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema mtuhumiwa wa tukio hilo anashikiliwa na jeshi la polisi kwa uchunguzi zaidi. Na JF
Joseph Mbilinyi amesema hayo baada ya kumtembelea Tundu Lissu jijini Nairobi nchini Kenya na kusema kutokana na uimara ambao Tundu Lissu anao amewataka Watanzania kujianda. " Nimemtembelea 'Big hommie', Nairobi hospital. Ameniambia nikawaambie wana Mbeya kuwa alisikia mwitikio wao wa kishindo nilipomtaja kwenye jukwaa la muziki na kuwa mwili wake 'uliovunjwa vunjwa' kwa risasi unazidi kuimarika na atasimama tena. Ameniagiza niwaambie wana Mbeya na Watanzania wote wajiandae, wajiandae, wajiandae " alisema Sugu. Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini,Mh. Joseph Mbilinyi pamoja na Mbunge wa Iringa Mjini juzi walimtembelea Tundu Lissu jijini Nairobi Kenya anapopatiwa matibabu kufuatia kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake mjini Dodoma Septemba 7, 2017.
Mtibwa Sugar imelazimishwa sare kye uwanja wake wa nyumbani hivyo kushindwa kukaa kileleni baada ya kufikisha alama 16 na kulingana na timu za Simba, Yanga na Azam FC. Mechi nyingine ni ile kati ya Kagera Sugar dhidi ya Ndanda FC ambapo Kagera Sugar imepata ushindi wake wa kwanza baada ya mechi 7, ikishinda mabao 2-1. Lipuli FC imeshinda mabao 2-1 dhidi ya Mbao FC. Njombe Mji ikiwa nyumbani imelazimishwa sare tasa na Stand United huku Majimaji ikitoka sare ya bao 1-1 na Mwadui FC. Kesho kutakuwa na mchezo mmoja wa kukamilisha raundi ya nane kati ya Tanzania Prisons dhidi ya Ruvu Shooting. Nafasi tano za juu kwenye msimamo zinashikiliwa na Simba yenye alama 16 ikifuatiwa na Yanga SC, Mtibwa Sugar na Azam FC zenye alama 16 pia. Singida United wanashika nafasi ya tano wakiwa na alama 13. Nafasi tatu za chini zinashikiliwa na Majimaji FC, Ruvu Shooting na Stand United zenye alama 5.
NIANZE kwa kumpa pole sana mama wa watoto watano, Zarinah Hassan ‘The Bossy Lady’ ambaye wiki chache zilizopita, alipata msiba mkubwa baada ya kufiwa na baba wa watoto wake watatu wakubwa, Ivan ‘Don’ Ssemwanga. Kwa namna yoyote, ule ni msiba mkubwa mno, hasa unapomkuta mwanamke, kwani inaonyesha wanaume, licha ya nao kuwa na moyo wenye damu unaoonja maumivu, angalau ni wavumilivu kidogo, wanaweza kujikaza na kusahau ndani ya muda mfupi. Zari, licha ya kuwa ni shemeji yetu, lakini pia ni mtu ambaye anaonyesha jinsi gani mwanamke anapaswa kuwa mtafutaji badala ya kumtegemea mwanaume kama dada zetu wengi walivyo. Ni mbunifu katika mipango ya kupata mkwanja, tena ule wa maana. Ameonyesha hivyo mara nyingi, kwani kwa muda mchache ambao amekuwa ‘mtu wetu’, amejidhihirisha kuwa ni wa tofauti na mastaa wetu ambao ujanja wao mwingi unategemea pochi za wanaume. Kuna ile Zari White Party, ni moja ya matukio machache kubuniwa na mdada huyo na kufanikiwa, likifanyika pale Mlimani City, miak...
Kuondoka kwa Neymar katika klabu ya soka ya Barcelona kunaweza kukawa kumemuumiza zaidi Lionel Messi ambaye amekuwa karibu zaidi na mchezaji huyo kwa takribani misimu minne. Messi kupitia mtandao wa Instagram, amemuandikia ujumbe wa kumuaga rafiki yake huyo ambaye anatarajiwa kukamilisha usajili wake wa kujiunga na PSG ya Ufaransa wiki hii kwa ada ya uhamisho utakaovunja rekodi ya dunia wa paundi milioni 198. “It was a great pleasure to have shared all these years with you, friend @neymarjr. I wish you good luck in this new stage of your life. See you tomorrow,” ameandika Messi katika mtandao huo.
Wabunge wa Chama tawala Nchini Uganda cha National Resistance Movement (NRM) cha Rais wa sasa wa nchi hiyo, Yoweri Museveni wamekubaliana kuwasilisha bungeni mswada wa kuondoa ukomo wa umri wa rais kutoka kwenye katiba ya nchi hiyo. Katiba ya Uganda kwa sasa hairuhusu mtu yeyote mwenye umri zaidi ya miaka 75 kugombea nafasi ya urais wa nchi hiyo ili kutoa wigo kwa vijana ambao bado wana nguvu za kuweza kulitumikia taifa lao. Aidha, Rais wa sasa wa nchi hiyo, Yoweri Museveni ana umri wa miaka 73, ambapo ni miongoni mwa viongozi waliotawala kwa muda mrefu zaidi barani Afrika na amekuwa madarakani kwa zaidi ya miongo mitatu. Hata hivyo, Uchaguzi Mkuu wa Urais nchini humo unatarajiwa kufanyika mwaka wa 2021 ambapo rais wa sasa atakuwa ameshavuka miaka kadhaa umri huo. Na dar24
Zifuatazo ni Picha za Madaraja [Bridges] yenye Ubora na Ukubwa hapa Duniani na yanapopatikanapo; 1. Danyang-Kunshan Grand Bridge(Daraja) Hili ni Daraja lenye urefu zaidi ya Kilometre 164 ;Linapatikana CHINA. 2.Tianjin Grand Bridge Urefu ni zaidi ya Kilometre 100 ; Mahali ni CHINA 3.Weinan Weihe Grand Bridge Urefu wa Daraja hilo ni Kilometre 79.7 ; Mahali CHINA 4.Bang Na Expressway Urefu wa Daraja hilo ni Kilometre 56 , Mahali THAILAND 5.Beijing Grand Bridge(Beautiful Bridge) Urefu wa Daraja hilo ni Kilometre 48 ; Mahali CHINA 6.Lake Pontchartrain Causeway Urefu wa Daraja hilo ni Kilometre 38.35 ; mahali U.S.A [MAREKANI] 7 .Manchac Swamp Bridge Urefu wa jumla ni Kilometre 36.69 ; Mahali U.S.A [MAREKANI] 8.YangCun Bridge Urefu wa Daraja hilo ni Kilometre 35.8 ; Mahali ni CHINA 9.Hangzhou Bay Brigde Ure...
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amepinga maamuzi ya Chama Cha Wananchi (CUF) kuwafukuza Uanachama Wabunge wawili wa chama hicho Magdalena Sakaya na Maftaha Nachuma na kusema Maalim Seif hatambuliki kama Katibu Mkuu wa CUF. Msajili wa Vyama vya Siasa amesema hayo leo wakati akijibu barua iliyowasilishwa ofisini kwake na Katibu Mkuu wa (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad akimtaka msajili wa vyama kuwavua nafasi ya Ubunge viongozi hao. Kufuatia barau hiyo Msajili wa Vyama Vya Siasa amesema kuwa hamtambui Maalim Seif Sharif Hamad kama Katibu Mkuu wa CUF na kusema yeye anawatambua Mwenyekiti wa CUF, Professa Ibrahim Lipumba pamoja na Magdalena Sakaya kama mtu mwenye dhamana ya Katibu Mkuu wa CUF Chama Cha Wananchi (CUF) kipo katika mgogoro wa pande mbili upande wa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif pamoja na upande wa Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Msajili wa Vyama Vya Siasa nchini Profesa Ibrahim Lipumba, kufuatia mgogoro huo mpaka sasa kuna kesi mbalimbali ambazo...
Muimbaji Lulu amekiambia kipindi cha Uhondo cha E Fm kuwa alitambua kuwa yeye ni mzuri kutokana na sifa alizokuwa akipewa na mama yake mzazi kitu ambacho kilimfanya kutolaghaika na watu waliokuwa wakimsifia. “Mimi ni msichana ambaye nipo sex ambaye nina mvuto, mama yangu alikuwa akiniambia Lulu mwanangu mashallah, yaani hapa sidhani kama kuna mtu nitamwambia idadi ya ng’ombe ninazozitaka halafu akapindua,” amesema na kuongeza. “Na mimi mwenyewe nikawa najiona ndio maana hata sikuweza kurubunika, yaani ile mtu kuniambia wewe mzuri akanidanganya kwa vichipsi mayai, mwenyewe nilishajijua ni mzuri,” amesema Lulu Diva. Hitmaker huyo wa Usimwache kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake inayokwenda kwa jina la Utamu.
Comments