Real Madrid wamewaambia Manchester United kuwa ikiwa wanahitaji kumsaini Gareth Bale 28, watalazimika kumuachia kipa David de Gea 26, ili ahamie Bernabeu. (Mirror) Meneja wa zamani wa Livepool Rafa Benitez huenda akahama Newcastle kujiunga na Everton ikiwa Ronald Koeman ataihama Everton. (The Sun) Mesut Ozil 28, na Alexis Sanchez wote wa Arsenal hawatakuwa na mikataba miwishoni mwa msimu na Arsenal inatakata kuwauza mwezi Januari. (Star) Itawalazimu Liverpool na Barcelona kumng'ang'ania mlinzi wa Southampton Virgil van Dijik, ikiwa wangependa kumsaini mwezi Januari. (Mirror) Everton wako tayari kutoa ofa ya pauni milioni 31 kwa mchezaji wa kiungo cha kati wa Sporting Lisbon, William Carvalho 25, licha ya klabu hiyo ya Ureno kusema kuwa haumuuzi. (Daily Mail, via Record) Mshambuliaji wa Everton Henry Onyekuru 20, amethibitisha kuwa alikutana na maafisa wa klabu yake wiki iliyopita kuzungumzia kurejea mapema kutoka kwa mkopo na klabu ya Anderlecht. (Liverpool Echo) Ars...
Aliyekuwa msimamizi msaidizi wa IEBC katika Uchaguzi Mkuu, Caroline Odinga amekutwa akiwa ameuawa baada ya kubakwa. - Mwili wake ulikutwa katika soko la Sega Jumamosi asubuhi na watu waliokuwa wakielekea katika mazishi ya Mkurugenzi wa TEHAMA wa IEBC, Chris Msando katika kijiji cha Lifunga. Na jamiiforum
Ni asubuhi nyingine tena nakukutanisha na habari kubwa kwenye Magazeti ya Tanzania leo September 30 2017 kua nzia ya Udaku, Michezo na Hardnews kujionea yote makubwa yaliyoandikwa
Muimbaji Lulu amekiambia kipindi cha Uhondo cha E Fm kuwa alitambua kuwa yeye ni mzuri kutokana na sifa alizokuwa akipewa na mama yake mzazi kitu ambacho kilimfanya kutolaghaika na watu waliokuwa wakimsifia. “Mimi ni msichana ambaye nipo sex ambaye nina mvuto, mama yangu alikuwa akiniambia Lulu mwanangu mashallah, yaani hapa sidhani kama kuna mtu nitamwambia idadi ya ng’ombe ninazozitaka halafu akapindua,” amesema na kuongeza. “Na mimi mwenyewe nikawa najiona ndio maana hata sikuweza kurubunika, yaani ile mtu kuniambia wewe mzuri akanidanganya kwa vichipsi mayai, mwenyewe nilishajijua ni mzuri,” amesema Lulu Diva. Hitmaker huyo wa Usimwache kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake inayokwenda kwa jina la Utamu.
Choirul Huda, mwenye miaka 38, alikimbizwa hospitalini siku ya Jumapili lakini muda mfupi baadae ilitangazwa kwamba amefariki dunia. Katika taarifa iliyotolewa na tovuti ya klabu yake Persela FC , daktari wa timu Yudistiro Andri Nugroho amesema mchezaji huyo alifariki baada ya kupata madhara makubwa kifuani. Anasema mgongano huo ulisababisha kushindwa kupumua kwa Huda. Ameongeza kuwa madaktari walijaribu kuokoa maisha yake bila mafanikio. Mchezo huo uliisha kwa Persela kuifunga Semen Padang 2-0. Maelfu ya mashabiki wamefika hospitalini alipofia mchezaji huyo aliyecheza michezo 500 ya ligi kuu kwa klabu yake pekee. Na BBC
UHALISI WA MAISHA: Maisha halisi ya mwanamke anayetarajia kuwa mke/ mke tayari hii ni kumaanisha kuwa wanawake mashujaa tunapaswa kuishi maisha ambayo yanatutambulisha kama mfano wa kuigwa ili tunapozungumza na kufundisha mabadiliko tuwe tunazungumza uhalisia wa maisha yetu ambao unajengwa na haya yafuatayo; UVUMILIVU: Kuwa mvumilivu katika maisha yake ya kila siku hasa ukizingatia kuwa tunakutana na mambo mbali mbali yasiyotuvutia katika mahusiano yetu, mengine ni magumu na yanayokwenda kinyume kabisa na matakwa yetu au mazoea yetu ya binafsi. Ifahamike kwamba wewe kama mwanamke shujaa inapotokea umekutana na mambo kama haya hupaswi kuonyesha hasira zako wazi wazi kama vile; chuki, kulaumu, ugomvi, vurugu, malalamiko, manung’uniko, machafuko, kulipa kisasi au aina yoyote ya uharibifu kutokea kwako au ndani mwako. Hivyo mwanamke shujaa huwa ni heri kila anapokuwa kwani hutunza amani ya eneo alipo. UPENDO WA DHATI: Maisha ya upendo wa halisi na sio wa kinafki kwa jamii inayomz...
Muigizaji Gabo Akiwa jana kwenye kipindi cha FNL cha EATV, Gabo aliweka wazi kuwa maneno ya kuzushiwa kati yake na malkia huyo wa filamu yalianza tu baada ya picha za wawili hao kuanza kusambaa ambazo zilikuwa zina mahadhi ya mapenzi na kuwejka wazi kuwa zilikuwa zimebeba maudhui ya filamu. " Mimi na Wema ni kazi tu. Hakuna kitu cha tofauti ambacho tulikifanya au tulikianzisha tukiwa location kwa sababu mpenzi wake alikuwa anakuja nae mara zote ambazo tulikuwa tuna shoot. vipande vyote alikuwa na sisi bega kwa bega sasa hata kama ni hayo mahusiano tungeyaanzisha muda gani? Watu wasifikiri tofauti kwani ukaribu wangu na Wema Sepetu umezalisha filamu ya Kisogo ambayo tunaamini watanzania wataifurahia" alisema Gabo Gabo Zigamba akiwa na muigizaji Wema Sepetu Aidha Gabo amezungumzia filamu yake mpya kwa kusema amefanya tofauti kabisa na ilivyozoeleka kuwa na filamu ndefu yenye maudh...
Dar es Salaam. Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Abdulla Juma Saadalla ‘Mabodi’ amesema CCM itaendelea kufanya ushindani wa sera za maendeleo zitakazowanufaisha wananchi wa makundi yote mijini na vijijini. Kauli hiyo ameitoa leo (Jumamosi) wakati akifungua mafunzo ya Wanawake na Uongozi kwa wanachama na viongozi wa Umoja wa Wanawake (UWT), Mkoa wa Mjini huko Amani Zanzibar. Dk Mabodi amesema wananchi wa Zanzibar kwa sasa wanachohitaji ni siasa za ushindani wa kisera katika kukuza kipato cha mwananchi mmoja mmoja hadi taifa kwa ujumla. Amesema taifa lolote linalotamani kuendelea kiuchumi ni lazima wananchi wake wakubali kwa vitendo dhana ya siasa za ustaarabu katika kudumisha amani na utulivu wa nchi ili kufanya kazi za kujiongezea kipato na kukuza uchumi wa nchi. #mwananchi
Serikali imewataka wananchi kupuuza uvumi ulianzishwa na wanasiasa juu ya ndege za Bombadier na kusema kuwa wawe watulivu ndege ya tatu ipo na inakuja nchini hivyo waendelee kuiamini serikali yao. Hayo yamesemwa na Ndg. Zamaradi Kawawa Kaimu Mkurugenzi mkuu idara ya habari "Kuhusiana na mgogoro wa ununuzi wa ndege hatua za Kidiplomasia na sheria zimeanza kuchukuliwa ili kumaliza jambo hili" -
Mwanamke mmoja nchini Kenya ameamua kuingia mtaani kusaka mume huku akiwa amebeba bango katikati ya jiji la Nairobi. Akiwa amevalia nguo nyeupe- kama ya harusi- mwanamke huyu mwenye umri wa miaka 28, Pris Nyabura, amebeba bango linalosema: “Nahitaji mume, nina mtoto wa kike wa miaka saba.” Mwandishi amejaribu kumpigia simu ili kupata taarifa zaidi, lakini simu yake iko “bize”….
Comments