Uchumi wa taifa la Korea Kaskazini uliimarika kwa haraka katika kipindi cha miaka 17 iliopita licha ya kuwekewa vikwazo kutokana na mpango wake wa kinyuklia na utengenezaji wa makombora ya masafa marefu. Uzalishaji wa bidhaa nchini humo ulikuwa kwa asilimia 3.9 2016 ikilinganishwa na mwaka uliopita kulingana na benki ya Korea. Ukuwaji huo unatokana na uchimbaji madini, kawi na uuzaji wa bidhaa nchini China. Marekani imekuwa ikiitaka Beijing kukata biashara na Pyongyang huku wasiwasi ukiongezeka kuhusu mipango ya kinyuklia ya rais Kim Jong Un. China ndio mshirika pekee mkuu wa Korea Kaskazini na mfadhili mkubwa wa misada nchini humo. Wiki iliopita China ilitoa data ikidai kuwa Korea Kaskazini haina uwezo mkubwa kama inavyodaiwa na rais Trump. Lakini huku Beijing ikisitisha ununuzi wa mkaa kutoka Korea Kaskazini, imeendelea kufanya biashara ya chuma na bidhaa nyengine. Ijapokuwa Korea Kaskazini haichapishi data za kiuchumi , benki kuu ya Korea Kusini inatoa takwimu za uk...
Stori:Waandishi Wetu | IJUMAA WIKIENDA Kilimanjaro: Ni wiki moja imekatika sasa tangu shujaa wa demokrasia aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk Philemon Kiwelu Ndesamburo ‘Ndesa Pesa’ azikwe nyumbani kwake, Mtaa wa KDC, Barabara ya Mbokomu, nje kidogo ya Mji wa Moshi. Nyuma ya kifo cha Ndesa Pesa aliyefariki dunia ghafla akiwa ofisini kwake mjini Moshi, akiwa na umri wa miaka 82, mambo mengi mazuri aliyoyafanya yangali yanazungumzwa, ikiwemo utajiri aliouacha, jambo ambalo linalisukuma Wikienda kutafuta undani wake na hapa linakuletea ripoti kamili ya utajiri wa kutisha wa Ndesa Pesa. HOTELI ZA KITALII HADI LONDON Kwa mujibu wa mmoja wa watoto wa Ndesa Pesa ambaye hakutaka kuandikwa gazetini, miongoni mwa vitega uchumi vya baba yake ni pamoja na hoteli za kitalii zilizopo katika Jiji la London, Uingereza, Kariakoo jijini Dar es Salaam na mjini Moshi. Baadhi ya hoteli hizo, mbili kubwa zipo mkoani Kilimanjaro maeneo...
Acacia imeona matokeo ya kushtua ya kamati ya pili ya Rais iliyowasilishwa kwa Rais wa Tanzania Mh. Dk John P. Magufuli leo asubuhi ambayo imeangalia nyanja za historia za kiuchumi na kisheria ya mauzo ya nje ya makanikia ya madini. Kamati ya Pili imetoa matokeo yake kwa kutumia matokeo ya Kamati ya Rais ya Kwanza, iliyotangazwa tarehe 24 Mei 2017, ambayo Acacia imeikanusha vikali. Kamati hiyo ilipata matokeo yake kwa kutumia sampuli ya kontena 44. Kwa mujibu wa data za zaidi ya miaka 20 tulizonazo ni vigumu kuoanisha matokeo yetu na yaliyokutwa na kamati, na kamati imetoa thamani ya juu kwa zaidi ya mara 10 kuliko thamani halisi ya makanikia Kamati ya Pili inadai kuwa Acacia imetangaza kiasi cha chini cha mapato kuliko inavyopata na kulipa kodi kidogo kuliko inavyostahili kwa miaka mingi na kuficha mabilioni ya dola ya Marekani. Na hivyo imefanya mapendekezo kadhaa ikiwa ni pamoja na Acacia kulipa kodi inayodaiwa na mirahaba, kufanya majadiliano upya ya mikataba miku...
Serikali ya Israel imetangaza kuondoa vifaa maalumu vya ukaguzi kwenye eneo takatifu la msikiti wa Jerusalem, ikisema haitatumia tena vifaa hivyo baada ya kuzusha sintofahamu mwishoni mwa juma kati ya waumini na vikosi vya Serikali. Uamuzi huu umekuja wakati huu jumuiya ya kimataifa ilikuwa inafanya juhudi kuzuia vurugu kwenye ardhi ya Palestina, huku utawala wa Israel ukisema utatumia mbinu nyingine za kiusalama baada ya juma moja lililopita wanajeshi wake wawili kuuawa kwenye msikiti wa Al-Aqsa. Maofisa wa kiislamu bado hawajaamua ikiwa wakubaliane na hatua ya Israel au la ili wasitishe mgomo wao wa kutotumia msikiti huo kusalia ambao unatumiwa pia kama kanisa na raia wa kiyahudi. Timu maalumu ilifanya kazi ya kuondoa vifaa maalumu vya utambuzi kwenye geti kuu la kuingilia kwenye msikiti huo na hata kamera zilizokuwa zimewekwa kwenye eneo hilo pia nazo ziliondolewa. Mamia ya wanajeshi wa Israel hata hivyo walisalia kwenye lango kuu la kuingilia kwenye msikiti huo, eneo amb...
Muimbaji Lulu amekiambia kipindi cha Uhondo cha E Fm kuwa alitambua kuwa yeye ni mzuri kutokana na sifa alizokuwa akipewa na mama yake mzazi kitu ambacho kilimfanya kutolaghaika na watu waliokuwa wakimsifia. “Mimi ni msichana ambaye nipo sex ambaye nina mvuto, mama yangu alikuwa akiniambia Lulu mwanangu mashallah, yaani hapa sidhani kama kuna mtu nitamwambia idadi ya ng’ombe ninazozitaka halafu akapindua,” amesema na kuongeza. “Na mimi mwenyewe nikawa najiona ndio maana hata sikuweza kurubunika, yaani ile mtu kuniambia wewe mzuri akanidanganya kwa vichipsi mayai, mwenyewe nilishajijua ni mzuri,” amesema Lulu Diva. Hitmaker huyo wa Usimwache kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake inayokwenda kwa jina la Utamu.
Klabu ya Real Madrid yanyakua kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuinyuka Juventus kwa mabao 4 kwa 1. - Inakuwa klabu ya kwanza kufanya hivyo, huku Kocha Zidane akiweka rekodi ya kuingoza klabu hiyo kushinda Mara 2 mfululizo. - Cristiano Ronaldo aibuka mfungaji bora wa michuano baada ya kufunga magoli 12
Katika hali isiyo ya kawaida Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, amedai kwamba kumekuwapo na jaribio la kutaka kumuua kwa sumu kwa kumtumia mtu wake wa karibu mno. Zuma ameibua madai hayo huku uvumi unaohusisha jina la mmoja wa wake zake ukisambaa ingawa yeye binafsi, licha ya kuthibitisha kuwapo kwa jaribio hilo, amekwepa kutaja moja kwa moja jina la muhusika. Mkewe anayetajwa kuhusishwa katika njama hizo Nompumelelo Ntuli Zuma maarufu kwa jina la “Ma Ntuli” ambaye ni mke wa pili wa kiongozi huyo ambaye hivi karibuni alinusurika kung’olewa katika kiti cha urais baada ya kura alizopigiwa za kutokuwa na imani naye bungeni kutotosha. “Nusura nife kwa sababu waliniwekea sumu, walifanikiwa kumpa mtu aliyekuwa karibu mno nami na hili nalijua fika,” alidai Zuma bila ya kutaja huyu muhusika katika tukio hilo. Kwa mujibu wa kiongozi huyo mwenye kupenda kuendeleza utamaduni mashuhuri barani Afrika wa kuoa wake wengi, amenusurika kuuawa kwa kuwekewa kiwango kikubwa cha sumu kiasi cha kuwash...
Wengi wamejikuta wakiitwa wahuni kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na makundi ya wanaume au wanawake. Hata hivyo wachunguzi wa masuala ya mapenzi wanasema idadi kubwa ya wapenzi si kigezo sahihi cha kupima tabia ya mtu na kumhusisha na uhuni. Watalaam hao wanataja safari ya kupata chaguo halisi la mwanaume/mwanamke wa maisha ndiyo inayowaponza wengi kiasi cha kujikuta wameingia katika kashfa ya kuwa na uhusiano na dazeni ya wapenzi. Wanasema msichana/mvulana anayeingia katika uwanja wa mapenzi kwa kuwa na hisia za kufanya ngono, hukosa umakini wa nani anafaa kuwa mpenzi wake kutokana na kukosa elimu ya uhusiano kutoka kwa wazazi wake. Kwa mantiki hiyo, bila upembuzi wa kina, mtu asiye na elimu ya jinsi ya kumpata mpenzi wa kweli hujikuta ameangukia kwa mwanaume/mwanamke asiyemfaa, ambapo baadaye huamua kuachana na huyo na kwenda kwa mwingine kujaribu bahati tena ya kupata penzi la kweli. Zinatajwa zawadi, hitaji la kusaidiwa kimaisha, mvuto wa kimahaba na mazoea kuwa ni ...
Askari wasiopungua tisa na raia wawili walikatwa vichwa siku ya Jumatano nchini Libya katika shambulio lililodaiwa kutekelezwa na kundi la Islamic State dhidi ya ngome ya majeshi yanayomtii Marshal Khalifa Haftar. Shambulio hilo lilifanyika mapema alafajiri katika eneo la al-Joufra, kilomita 500 kusini mwa Tripoli, kwa mujibu wa Kanali Ahmed al-Mesmari, msemaji wa kundi la wapiganaji wa NLA linalomtii Marshal Haftar. Siku ya Jumatano alasiri, kundi la Islamic state lilidai kutekeleza shambulio hilo katika taarifa iliyotolewa na shirika lake la propaganda la Qama. Anadai kuwa aliua na kujeruhiwa "wanamgambo 21 wa Haftar" katika shambulio la "wapiganaji wa IS" kusini mwa al-Joufra. Wapiganaji wa kundi la NLA walikua walidhibiti eneo hilo mapema mwezi wa Juni. Lakini mapigano yanaendelea kati ya makambi mawili karibu na wilaya ya Soug al-Hout. Na Rfi
Comments