ubingwa wa dunia mikononi mwa Hamilton

Hata hivyo Hamilton ana nafasi ya kufanya hivyo baada ya kujihakikishia nafasi ya kwanza kwenye mpangilio wa magari wakati wa mbio hizo. Mkali huyo wa gia kutoka nchini Uingereza ameongoza mbio za kusaka nafasi kwenye kupanga magari ambapo sasa leo ataanza wa kwanza.
Mpinzani wake wa karibu Sebastian Vettel kutoka timu ya Ferrari amemaliza wa pili hivyo gari yake itasimama kwenye nafasi ya pili wakati wa mbio za USGP leo akifuatiwa na gari ya Valtteri Bottas wa Mercedes ambaye atakuwa wa tatu.
Mbio zitafanyika jioni ya leo kwenye mitaa ya Austin jijini Texas Marekani. Hadi sasa Lewis Hamilton anaongoza mbio hizo akiwa na alama 306 mbele ya Sebastian Vettel mwenye pointi 247.
Baada ya mbio za leo za USGP zitakuwa zimebaki mbio 3 ili kumaliza msimu wa 2017 ambazo ni Mexico Grand Prix, Brazilian Grand Prix na Abu Dhabi Grand Prix.

Comments


Popular posts from this blog

Nape Nnauye ameweka video ya Pius MsekwaMsekwa nakusema haya

mimi nipo sex Lulu diva

Cristiano Ronaldo kawaonesha watoto wake mapacha leo

Mchawi wa Bongo Movie ni Sisi Wenyewe

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO

Hii ndiyo Nyumba aliyonunua Barack Obama

, Tundu Lissu akiwa sambamba na Dkt. HEllen Kijo-Bisimba

msuva ageuka lulu dau la usajili lapanda hadi........