Wanawake wazidi kuikimbia Sudan kusini


Maelfu ya wanawake na watoto kutoka Sudan kusini wamevuka mpaka kuingia nchini Sudan tangu kuanza kwa mwaka huu, wakikimbia ghasia na kitisho cha njaa.
Kwa mujibu wa Shirika la Kuwahudumia Wakimbizi Duniani -UNHCR- Karibu Wasudan kusini laki moja na 37 elfu wameingia nchini Sudan tangu Januari mosi, huku wengine zaidi ya laki moja na 31 elfu wakiwa tayari wamewasili nchini humo tangu mwaka 2016.
Wafanyakazi wa misaada wanaarifu kuwa wengi ya watu hao wanaowasili sasa ni wanawake na watoto.
Mkurugenzi wa Shirika la Msalaba mwekundu, kanda ya Afrika Dokta Faroumata Nafo-Traore wengi wanakuwa wamedhoofika kiafya na wamekuwa na msongo wa mawazo kutokana na hali iliyowatokea huko wanakotoka.
Tangu Desemba mwaka 2013 jumla ya wakimbizi laki nne na 17 elfu wa Sudan Kusini waliingia nchini Sudan. Wengi wao wako katika kambi zilizokuwa Mashariki na Kusini mwa Darfur na magharibi na kusini mwa KordofanxKordofanx
Habari na BBC

Comments


Popular posts from this blog

ILE SINTOFAHAMU YA NANI BINGWA WA VPL HII HAPA

Michezo:Ajibu huyo yanga

ELIZABETH MICHAEL ' LULU' awafungukia wasanii wa bongo move

KUTOKA IKULU:Rais Magufuli amefanya uteuzi mwingine leo julai 6 2017

fahamu kilichojiri nyumbani kwa Tundulisu