Mfalme wa Saudia amfuta kazi mrithi wake.


Mfalme Salman wa Saudia amebadilisha mkondo wa urithi na kumfanya mwanawe wa kiume Mohammed bin Salman kuwa mwanamfalme na kuwa wa kwanza kumrithi.
Aliyekuwa mwanamfalme Mohammed bin Nayef amepokonywa taji lake na kufutwa kazi kama waziri wa maswala ya ndani.
Mohammed bin Salman mwenye umri wa miaka 31 ataendelea kuwa waziri wa ulinzi mbali na kuwa naibu waziri mkuu.
Rais Bashir akataa kuonana na Trump Saudia
Trump azuru Saudia, huku joto la kisiasa likimkabili nyumbani
Mwanamfalme akatwa shingo Saudi Arabia
Mabadiliko hayo yalitangazwa katika misururu ya amri za kifalme.
Chombo cha habari cha Saudia kimesema kuwa mfalme ametaka raia wa taifa hilo kumtii mwanamfalme huyo mpya siku ya Jumatano.
Hatua ya kumpa cheo hicho Salman iliidhinishhwa na wanachama 31 kati ya 34 wa baraza kuu.
Wadadisi wanasema kuwa wale walio madarakani hupenda kuwateua watoto wao wa kiume kwa nafasi ambazo zitawawezesha kupandishwa vyeo.
Mfalme Salman ambaye ni mtoto wa Mfalme Abdulaziz alishika hatamu za uongozi mwaka 2015 baada ya kifo cha ndugu wa kambo Abdullah bin Abdul Aziz.
Iran 'yapuuzilia mbali' taarifa ya Trump kuhusu shambulio la Tehran
Alifanya mabadiliko makubwa kwa baraza lake la mawaziri miezi michache baadaye na kumpandisha cheo Mahammed bin Nayef kuwa mrithi na Mohammed bin Salam ambao wakati huo hawakuwa na umaarufu.
chanzo BBC

Comments


Popular posts from this blog

Uchumi wa taifa la Korea Kaskazini waimarika

harakati za ndesamburo na utajiri wake hizihapa

ACACIA wapinga vikali matokeo ya kamati ya pili ya Rais

IsraelIsrael yasalimu

mimi nipo sex Lulu diva

Real madrid mabingwa tena UEFA

Rais Zuma akiri kunusurika kuuawa kwa sumu

Hatua 10 Muhimi za Kumchagua Mchumba Mtakae Funga Ndo. a tzaama SOMA NA SHARE HII

Watu kumi na mmoja wauawa katika shambulio