MANARA AMKABIDHI JPM KIWANDA


Mkuu wa habari na mawasiliano wa klabu ya Simba, Haji Manara amemuonesha Rais Magufuli kiwanda kingine ambacho amedai kuwa ni kikubwa kuliko viwanda vyote nchini kinachoweza kusaidia utekelezaji wa kauli mbiu ya serikali ya awamu ya tano ya kujenga Tanzania ya viwanda.


Kiwanda hicho ni mchezo wa soka, ambapo Manara amesema endapo kitafanyiwa uwekezaji wa kutosha kitaweza kuzalisha ajira nyingi kuliko viwanda vyo ambavyo serikali ya awamu ya tano imepanga kuvijenga na kuviendeleza.

“TFF wanatakiwa waje na mpango wa kukiboresha na kukiunda kiwanda hiki sasa, maana mimi naona kama vile kiwanda hiki hakipo, serikali iwekeze kwenye football kuanzia chini. Kama Rais ameingia mahali, nchi nzima inatumia mashine za EFD, TRA makusanyo yameongezeka, ofisini kuna nidhamu ya kazi kwenye taasisi za umma, mambo yanakwenda, nakuhakikishia Rais akiingia hapa kwenye mpira, akaja kutuundia hiki kiwanda, ataacha legacy ambayo hajaacha Rais yeyote, na kisiasa itamsaidia sana katika uchaguzi wa 2020, kwa sababu hakuna kitu kinachopendwa zaidi katika nchi hii kama mpira” Amesema Manara.

Na. Azamtv

Comments


Popular posts from this blog

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI 27.08.2017

Maajabu ya pacha walioungana, wajikuta katika penzi moja .

Picha sita 6 mende wamaajabu duniani

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 31.08.2017

TANZIA: Aliyewahi kuwa mbunge wa Moshi Mjini, Mzee Philemon Ndesamburo(CHADEMA) aaga dunia

Picha ya Beckham na mtoto wake Serengeti imeleta mjadala hadi kwao

MTWARA:watu watano wanashikiliwa na Jeshi la polisi

Jux afunguka haya kuhusu vanessa mdee

Marekani yatishia vikwazo kwa yeyote atakaekwamisha uchaguzi DRC