Stori:Waandishi Wetu | IJUMAA WIKIENDA Kilimanjaro: Ni wiki moja imekatika sasa tangu shujaa wa demokrasia aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk Philemon Kiwelu Ndesamburo ‘Ndesa Pesa’ azikwe nyumbani kwake, Mtaa wa KDC, Barabara ya Mbokomu, nje kidogo ya Mji wa Moshi. Nyuma ya kifo cha Ndesa Pesa aliyefariki dunia ghafla akiwa ofisini kwake mjini Moshi, akiwa na umri wa miaka 82, mambo mengi mazuri aliyoyafanya yangali yanazungumzwa, ikiwemo utajiri aliouacha, jambo ambalo linalisukuma Wikienda kutafuta undani wake na hapa linakuletea ripoti kamili ya utajiri wa kutisha wa Ndesa Pesa. HOTELI ZA KITALII HADI LONDON Kwa mujibu wa mmoja wa watoto wa Ndesa Pesa ambaye hakutaka kuandikwa gazetini, miongoni mwa vitega uchumi vya baba yake ni pamoja na hoteli za kitalii zilizopo katika Jiji la London, Uingereza, Kariakoo jijini Dar es Salaam na mjini Moshi. Baadhi ya hoteli hizo, mbili kubwa zipo mkoani Kilimanjaro maeneo...
Comments