Jux afunguka haya kuhusu vanessa mdee


Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Jux amesema Vanessa sasa hivi yupo kwenye wakati mgumu katika kufanya mambo yake ya kawaida, hivyo ni jukumu lake kuhakikisha haeleweki vibaya mbele za watu.
“Kuna vitu mimi siwezi kuvifanya ili kumlinda na yeye hawezi kufanya kunilinda mimi, japo watu watasema vingi hasa kwa mwanamke pale anapoamua kufanya baadhi ya vitu vyake binafsi. Natakiwa kumlinda Vanessa sasa hivi kwa kuwa kila jambo ambalo atalifanya watu watamfikilia vibaya hivyo napaswa kumlinda kutokana na hilo kwa sababu wanawake wenyewe wako wachache”, alisema Jux.
Jux aliendelea kwa kusema kuwa wakati bado wako kwenye mahusiano Vanessa alikuwa na uhuru wa kufanya jambo lolote, kwani karibia kila mmoja aliamini yupo na Jux ndiye mtu wake.
“Muda mwingine anaweza akashindwa hata kufanya vitu vingine, mwanzo hata akionekana na mtu wana-shoot au wanafanya nini, wanajua yupo na Jux, lakini sasa hivi hawezi”, alisema Jux
Pia Jux aliweka wazi kuwa ingawa bado ana kidonda cha maumivu ya kuachana na mpenzi wake huyo, lakini haikuwa ngumu kwao kufikia uamuzi huo, kwani kabla ya kuanza mahusiano walikuwa marafiki wa kawaida, kitu ambacho mpaka sasa bado wanacho.

  Na eatv

Comments


Popular posts from this blog

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI 27.08.2017

Maajabu ya pacha walioungana, wajikuta katika penzi moja .

Picha sita 6 mende wamaajabu duniani

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 31.08.2017

TANZIA: Aliyewahi kuwa mbunge wa Moshi Mjini, Mzee Philemon Ndesamburo(CHADEMA) aaga dunia

Picha ya Beckham na mtoto wake Serengeti imeleta mjadala hadi kwao

MTWARA:watu watano wanashikiliwa na Jeshi la polisi

MANARA AMKABIDHI JPM KIWANDA

Marekani yatishia vikwazo kwa yeyote atakaekwamisha uchaguzi DRC