Lema afunguka haya kuhusu utekaji wa watoto


Mh. Lema amesema matukio hayo ni mabaya na kwamba yanaleta taharuki na huzuni kwa wazazi na walezi hivyo ni vyema polisi wakachukua hatua za haraka kuwabaini watu wanaotekeleza vitendo hivyo na kuvikomesha.
Mbunge huyo amesema watekaji hao mara baada ya kuwateka watoto wanadaiwa kutoa barua za madai ya fedha kwa kificho ili wawaachie watoto na kwamba, endapo madai yao hayatakelezwa hutishia kuwaua.
Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Olkerian, Daudi Safari, amesema wasiwasi umezikumba familia nyingi kufuatia matukio hayo hali iliyosababisha wazazi na walezi kushindwa kutekeleza majukumu yao mengine wakitumia muda mwingi kuwalinda watoto wao.
Mpaka sasa watoto wanaodaiwa kutekwa nyara ni Maurine David, Ikram Salim, Ayoub Fred Bakari Salim. Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha kuzungumzia matukio hayo zimegonga mwamba

Comments


Popular posts from this blog

Afariki kwakuchomwa na kisu

Prof. Maghembe atoa neno kwa wavamizi wa misitu.

Wabunge wanamna hii kufukuza ccm

Maajabu ya pacha walioungana, wajikuta katika penzi moja .

Mtanzania aliyekataa mshahara wa Tsh. milioni 425 Marekani amerejea nyumbani

Barcelona sasa yawa moto baada ya hili

Mwanamke yeyote nampenda, awe mweusi, mweupe, mwembamba au unene – Timbulo

Mtandao wa biashara ya ngono wavunjwa

Kenyata sina matakwa yoyote kutoka IEBC

Mwezi Mtukufu… Roma Awafuturisha Watoto Yatima