Lema afunguka haya kuhusu utekaji wa watoto


Mh. Lema amesema matukio hayo ni mabaya na kwamba yanaleta taharuki na huzuni kwa wazazi na walezi hivyo ni vyema polisi wakachukua hatua za haraka kuwabaini watu wanaotekeleza vitendo hivyo na kuvikomesha.
Mbunge huyo amesema watekaji hao mara baada ya kuwateka watoto wanadaiwa kutoa barua za madai ya fedha kwa kificho ili wawaachie watoto na kwamba, endapo madai yao hayatakelezwa hutishia kuwaua.
Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Olkerian, Daudi Safari, amesema wasiwasi umezikumba familia nyingi kufuatia matukio hayo hali iliyosababisha wazazi na walezi kushindwa kutekeleza majukumu yao mengine wakitumia muda mwingi kuwalinda watoto wao.
Mpaka sasa watoto wanaodaiwa kutekwa nyara ni Maurine David, Ikram Salim, Ayoub Fred Bakari Salim. Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha kuzungumzia matukio hayo zimegonga mwamba

Comments


Popular posts from this blog

DROO YA KLABU BINGWA ULAYA HII HAPA

Nyumba ya Mbunge Kigoma Mjini Zitto Kabwe yaungua moto

Cristiano Ronaldo kawaonesha watoto wake mapacha leo

Baada ya Kifo cha Mumewe… Zari Akwaa Aibu 5 #Tazama

hali ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu

Wapiga dili wa madini sasa kukiona

Irine Uwoya: afunguka kuhusu ombi la Dogo Janja kummiliki

hii ndio furaha ya Diamond na zari