Mahanga akamatwa na Polisi

Dar es Salaam. Mbunge wa zamani wa Ukonga na Segerea, Dk Makongoro Mahanga amekamatwa na Polisi Mkoa wa Ilala kwa amri ya Mahakama Kuu na amefikishwa mahakamani.
Mahakama iliamuru Dk Mahanga akamatwe na kufikishwa mahakamani kwa kushindwa kutekeleza uamuzi unaomtaka amlipe mdai Kainerugaba Msemakweli Sh14 milioni.
Fedha hizo ni gharama za kesi alizozitumia Msemakweli baada ya kushinda kesi ya madai ya kashfa ambayo Dk Mahanga alimfungulia kwa kumtaja kwenye kitabu chake kinachoitwa: “Mafisadi wa Elimu”.
Katika kitabu hicho anamtaja kuwa ni mmoja wa viongozi wenye shahada za udaktari wa kughushi.
Kati ya kiwango hicho cha fedha, Dk Mahanga ameshalipa Sh6 milioni hivyo anadaiwa Sh8 milioni.
 Na mwananchi

Comments


Popular posts from this blog

Mwezi Mtukufu… Roma Awafuturisha Watoto Yatima

Baada ya Kifo cha Mumewe… Zari Akwaa Aibu 5 #Tazama

Picha 10:madaraja makubwa na bora duniani

Wakili anayemtetea Mwanafunzi Abdul Nondo ameyasema haya

mimi nipo sex Lulu diva

Mchungaji Lusekelo ameandika ujumbe huo kwa jamii kuusu Tundulisu

Mara: Aua wawili nakujijeruhi