Ni asubuhi nyingine tena na habari kubwa kwenye Magazeti ya Tanzania March 18 2018 kuanzia ya, Udaku, Michezo na Hardnews kujionea yote makubwa yaliyoandikwa
Liverpool wameweka makataa ya hadi Jumatatu, kwa Barcelona wawe wamefikia bei ya Philippe Coutinho, 25. (Onda Cero) Liverpool wanataka kukamilisha usajili wa Alex Oxlade Chamberlain, 24, kabla ya dirisha la usajili kufungwa. Chelsea pia wanamtaka winga huyo wa Arsenal. (Sunday Mirror) Mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28, imeripotiwa anaitaka klabu yake kumfanya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi katika EPL iwapo wanataka asaini mkataba mpya. (Daily Star) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger hajakata tamaa ya kumsajili Thomas Lemar wa Monaco, 22, pamoja na Virgil van Dijk, 26, ingawa huenda ikawa msimu ujao. (Sun) Arsenal wanataka kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Marco Asensio, 21. (Sunday Express) Paris Saint-Germain wanaendelea na majadiliano ya kumsajili mshambuliaji wa Monaco Kylian Mbappe kwa pauni milioni 166 kabla ya dirisha la usajili kufungwa, ingawa Monaco wenyewe wanataka Mbappe aende Real Madrid. (Sunday Telegraph) Iwapo Kylian Mbappe ataondoka Monac...
Mwandishi wa Mwananchi Tumaini Msowoya na Mkuu wa Kituo cha Nyota ya Asubuhi, Sister Idda Luizer wakiwa na mapacha, Maria na Consolata By Tumaini Msowoya, Mwananchi tmsowoya@mwananchi.co.tz Jana tuliishia sehemu inayoeleza jinsi pacha hawa walioungana, Maria na Consolata, wanavyochangia hisia za baadhi ya viungo vyao. Pengine ni kuchangia huko kwa hisia za viungo, kumefanya wawe pia na hisia moja katika masuala ya kimaisha. Wawili hawa wanahisia moja ya kimapenzi. Sasa endelea… Si rahisi kufikiria maisha ya ndoa ya Maria na Consolata kwa jinsi walivyo, lakini pacha hawa walioungana wako wazi kuhusu matamanio yao ya maisha ya ndoa. Katika mazungumzo yao na gazeti hili, Maria na Consolata waliweka bayana mipango yao ya ndoa mara watakapomaliza elimu ya chuo kikuu. Ingawa ni kitu cha kushangaza, Maria na Consolata hawatakuwa mapacha wa kwanza katika maisha ya ndoa. Chang na Eng Bunker ni pacha wanaume waliozaliwa mwaka 1811 nchini Thailand ambako zamani kuliitwa Siame. ...
Mende huyu anayepatikana nchini Japan na mwalimu wake ni aina ya mende wanaopatikana barani Asia, wanaotajwa kuwa kwenye hatari ya kuangamia Mende huyu anayepatikana nchini Japan na mwalimu wake ni aina ya mende wanaopatikana barani Asia, wanaotajwa kuwa kwenye hatari ya kuangamia Mende huyo alipata umaarufu mitandaoni wakai picha za michoro yake zilisambaa katika mtandoa wa Twitter Akiwa na kalamu zenye rangi mende huyo aliweza kuchora michoro tofauti Michoro hiyo imewavutia wengi mitandaoni na hata kusababisha kutangazwa kuuzwa kupitia Ebay Mende wa aina hii ni maarufu miongoni mwa watoto chini Japan Mende hawa ni kati wa wadudu wenye nguvu nyingi zaidi duniani Mdudu huyu na uwezo wa kupanda ukuta na pia anatajwa kusaidia hata kwenye mapishi Mwenye mdudu huyu anaamini kuwa umaarufur wake utasaidia watu kuwapenda wadudu BBC
Arsenal wanafanya jaribio la dakika za mwisho kumsajili mshambuliaji wa Paris St-Germain Julian Draxler, 23, na wakimkosa watazuia uhamisho wa Alexis Sanchez, 28, kwenda Manchester City. (Daily Mirror) Manchester City watapanda dau la pauni milioni 70 taslimu kutaka kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28, na tayari wamepeleka kikosi chake cha wansheria na madaktari nchini Chile kwa ajili ya kukamilisha usajili huo. (Independent) Matumaini ya Manchester City ya kumsajili beki wa West Brom Jonny Evans, 29, bado ni ati ati, kwa sababu Eliaquim Mangala, 26, ambaye angehusika katika mkataba huo hataki kwenda West Brom. Arsenal na Leicester walipanda dau la pauni milioni 25 kumtaka beki huyo, lakini maombi yao yalikataliwa. (Daily Telegraph) Crystal palace wana matumaini ya kumsajili Eliaquim Mangala kutoka City kwa pauni milioni 23. (Sun) Swansea wanakaribia kumsajili kiungo wa Bayern Munich Renato Sanches kwa mkopo. (Guardian) West Ham wanapanga kumchu...
TANZIA: Aliyewahi kuwa mbunge wa Moshi Mjini, Mzee Philemon Ndesamburo(CHADEMA) aaga dunia Taarifa ambazo tumezipata za uhakika muda huu kutoka Mkoani Kilimanjaro aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Moshi Mhe Ndesamburo amefariki muda mfupi uliopita. Taarifa zaidi zitatolewa muda mfupi ujao. ========UPDATES Kwa masikitiko tunawatangazia kuwa, Mbunge Mstaafu wa Moshi Mjini na Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa kilimanjaro, Mhe.Pilemon Ndessamburo amefariki Dunia mapema hii leo. Katibu wa kanda ya Kaskazini Amani Golugwa ====== Mzee Philemon Kiwelu Ndesamburo alizaliwa February 19, 1935. Alikuwa mwanasiasa kupitia chama cha demokrasia na maendeleo(CHADEMA) pia kufadhili mambo mengi kupitia chama hicho. Mwaka 2000 alifanikiwa kuchaguliwa na wananchi wa Moshi mjini kuwa mbunge wao mpaka mwaka 2015 alipoamua kwa ridhaa yake kutogombea tena jimbo hilo.
SOKA ULAYA Jina la staa wa soka wa zamani wa kimataifa wa England David Beckham limezidi kuchukua headlines baada ya wiki hii kuonekana akiwa Tanzania katika hifadhi ya Serenget i akiwa pamoja na familia yake watoto wake wanne na mkewe Victoria. Beckham akimbusu mwanae wa mwisho Harper Seven mwenye umri wa miaka mitano wakiwa Serengeti. Ilijulikana kuwa Beckham yupo Tanzania baada ya kusambaa kwa video fupi akionekana Beckham na familia yake Airport Dar es Salaam , Beckham amepiga picha kadhaa na kuzipost instagram akiwa Serengeti lakini picha na mtoto wake wa mwisho Harper imekuwa topic. Picha aliyopiga David Beckham akimkiss mtoto wake Harper Seven katika lips baadhi ya mashabiki wanaomfollow wameonekana kuikosoa na kuona haipo katika maadili na wengine wakiona haina shida, mjadala ambao umeendelea hadi mtandao wa mirror.co.uk wa England ambapo ndio kwao na David Beckham kuandika mawazo ya mashabiki hao
Watu watano wanashikiliwa na Jeshi la polisi mkoani Mtwara kwa kosa la kumvamia na kumshambulia kwa mapanga Hakimu wa Mahakama ya wilaya ya Masasi Halfani Saidi Ulaya na kumsababishia kifo. Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi mkoa wa Mtwara Lukas Mkondya amesema hakimu huyo alivamiwa nyumbani kwake na watu watatu na kuanza kumshambua kwa mapanga sehemu za mikono na kichawani. Hata hivyo Kamanda amesema baada ya kuhojiwa watuhumiwa hao wamekiri kushiriki tukio hilo la kumvamia Hakimu kwa lengo la kulipiza kisasi baada ya kuwahukumu wenzao kwenda jela kwa kosa la kufanya ujambazi na kuwaomba wananchi wa mkoa wa Mtwara kutoa ushirikiano kwa wahalifu wa aina. Na ITV
Mkuu wa habari na mawasiliano wa klabu ya Simba, Haji Manara amemuonesha Rais Magufuli kiwanda kingine ambacho amedai kuwa ni kikubwa kuliko viwanda vyote nchini kinachoweza kusaidia utekelezaji wa kauli mbiu ya serikali ya awamu ya tano ya kujenga Tanzania ya viwanda. Kiwanda hicho ni mchezo wa soka, ambapo Manara amesema endapo kitafanyiwa uwekezaji wa kutosha kitaweza kuzalisha ajira nyingi kuliko viwanda vyo ambavyo serikali ya awamu ya tano imepanga kuvijenga na kuviendeleza. “TFF wanatakiwa waje na mpango wa kukiboresha na kukiunda kiwanda hiki sasa, maana mimi naona kama vile kiwanda hiki hakipo, serikali iwekeze kwenye football kuanzia chini. Kama Rais ameingia mahali, nchi nzima inatumia mashine za EFD, TRA makusanyo yameongezeka, ofisini kuna nidhamu ya kazi kwenye taasisi za umma, mambo yanakwenda, nakuhakikishia Rais akiingia hapa kwenye mpira, akaja kutuundia hiki kiwanda, ataacha legacy ambayo hajaacha Rais yeyote, na kisiasa itamsaidia sana katika uchaguzi...
Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Jux amesema Vanessa sasa hivi yupo kwenye wakati mgumu katika kufanya mambo yake ya kawaida, hivyo ni jukumu lake kuhakikisha haeleweki vibaya mbele za watu. “Kuna vitu mimi siwezi kuvifanya ili kumlinda na yeye hawezi kufanya kunilinda mimi, japo watu watasema vingi hasa kwa mwanamke pale anapoamua kufanya baadhi ya vitu vyake binafsi. Natakiwa kumlinda Vanessa sasa hivi kwa kuwa kila jambo ambalo atalifanya watu watamfikilia vibaya hivyo napaswa kumlinda kutokana na hilo kwa sababu wanawake wenyewe wako wachache”, alisema Jux. Jux aliendelea kwa kusema kuwa wakati bado wako kwenye mahusiano Vanessa alikuwa na uhuru wa kufanya jambo lolote, kwani karibia kila mmoja aliamini yupo na Jux ndiye mtu wake. “Muda mwingine anaweza akashindwa hata kufanya vitu vingine, mwanzo hata akionekana na mtu wana-shoot au wanafanya nini, wanajua yupo na Jux, lakini sasa hivi hawezi”, alisema Jux Pia Jux aliweka wazi kuwa ingawa bado ana kidon...
Serikali ya Marekani juma hili imetishia kuwawekea vikwazo wale wote watakaobainika wanakwamisha kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC. Kauli ya Marekani imekuja wakati huu mwishoni mwa juma lililopita mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini humo, CENI Corneil Nangaa alitangaza kuwa tume yake haiwezi kuandaa uchaguzi mkuu mwishoni mwa mwaka huu. Kuendelea kucheleweshwa kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa DRC huenda kukasababisha kuzuka kwa machafuko zaidi nchini humo ambapo katika maandamano ya mwaka jana mamia ya watu walipoteza maisha. Naibu balozi wa Marekani kwenye baraza la usalama la umoja wa Mataifa, Michele Sison amesema kuwa nchi yake iko tayari kutangaza vikwazo dhidi ya mtu au kundi la watu watakaobainika wanakwamisha kufanyika kwa uchaguzi huru na wa kidemokrasia. Nchi ya Marekani mwaka jana ilitangaza vikwazo kwa maofisa kadhaa wa juu wa Serikali ya DRC ikiwa ni pamoja na kuzuia mali na fedha zao na kuzuia raia wake kufanya biashara za wat...
Comments