Uchumi wa taifa la Korea Kaskazini waimarika
Uchumi wa taifa la Korea Kaskazini uliimarika kwa haraka katika kipindi cha miaka 17 iliopita licha ya kuwekewa vikwazo kutokana na mpango wake wa kinyuklia na utengenezaji wa makombora ya masafa marefu. Uzalishaji wa bidhaa nchini humo ulikuwa kwa asilimia 3.9 2016 ikilinganishwa na mwaka uliopita kulingana na benki ya Korea. Ukuwaji huo unatokana na uchimbaji madini, kawi na uuzaji wa bidhaa nchini China. Marekani imekuwa ikiitaka Beijing kukata biashara na Pyongyang huku wasiwasi ukiongezeka kuhusu mipango ya kinyuklia ya rais Kim Jong Un. China ndio mshirika pekee mkuu wa Korea Kaskazini na mfadhili mkubwa wa misada nchini humo. Wiki iliopita China ilitoa data ikidai kuwa Korea Kaskazini haina uwezo mkubwa kama inavyodaiwa na rais Trump. Lakini huku Beijing ikisitisha ununuzi wa mkaa kutoka Korea Kaskazini, imeendelea kufanya biashara ya chuma na bidhaa nyengine. Ijapokuwa Korea Kaskazini haichapishi data za kiuchumi , benki kuu ya Korea Kusini inatoa takwimu za uk...
Comments