Mbunge Gulamali aelezea Sababu za kufufuliwa kiwanda cha ‘Manonga Ginery’


Mbunge wa Jimbo la Manonga kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Seif Khamis Gulamali leo ametembelea kiwanda cha Manonga Ginery kinachohusika na kutengeneza pamba, kilichokuwa kimesimama kwa takribani miaka ishirini (20) bila ya kufanya kazi.
Mapema leo hii Mbunge Gulamali aliwasili katika eneo la kiwanda hicho, iliyopo Jimbo la Manonga Kata ya Choma akiwa pamoja na Mmiliki wa kiwanda hicho, ndugu Urvesh Rajan pamoja na viongozi wa Serikali za mitaa, wahandisi na mafundi wa viwanda.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea na kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hicho ili kianze kufanya kazi upya, baada ya kukaa kwa miaka kadhaa bila ya kufanya kazi, Mbunge Gulamali alisema, leo nimekuja kuoana maendeleo ya kufufuliwa wa kiwanda hichi ikiwa ni sehemu ya kutaka kutimiza tena ahadi yangu niliyo itoa kwa wanachi wa Igunga na Manonga kwamba lazima kiwanda cha Manonga Ginery, kianze kazi ili wananchi waweze kunufaika katika zao biashara ya pamba na wengine kupata ajira kwa kuendesha maisha na kukuza uchumi wa viwanda nchini.
” Leo nimekuja kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hiki ikiwa ni sehemu yangu ya ahadi niliyo itoa kwa wananchi wangu wa jimbo la Manonga pamoja na Igunga kwamba lazima kiwanda hiki kifanye kazi tena, ili biashara ya zao la pamba lirudi tena na wananchi na waweze kupata ajira katika kiwanda hichi pia kukuza uchumi wa nchi ya Viwanda.
” Kufufuliwa kwa kiwanda hiki ni fursa kubwa ya maendeleo kwa jamii ya wana Igunga na Manonga na hasa wakulima wa zao la pamba hata kwa wananchi wanao lilia ajira, hivyo fursa kwa sasa iko wazi, alisema Gulamali.
Hata hivyo Mbunge Gulamali alisema kuwa bila kumpa ujumbe mmiliki wa kiwanda hiki na kutompa matakwa ya wananchi basi ingekuwa sicho kilichotokea leo, kwahiyo nimetumia uongozi wangu kwaajili ya wananchi wangu ili kuona maendeleo yakiendelea tena katika swala kiwanda na kuona zao la pamba likirudi tenaa kwa kasi katika Jimbo la Igunga na Manonga.
Lakini pia Mbunge Gulamali amewataka wakulima wa zao la pamba kuanza kulima kwa kasi kilimo cha hicho kwa kuwa sasa kiwanda hiki kitaanza kufanya kazi, hivyo juhudi na jitihada zenu ndio itakayoweza kufanya kiwanda hiki kiendelee kwa kuwa nao wanategemea pamba toka kwenu na wao waweze kuuza kwa wafanya biashara wakubwa wa nje ya mipaka na ndani ya nchi.
Hata hivyo Mmiliki wa kiwanda hicho, ndug, Urvesh Rajan amemshukuru Mbunge Gulamali sambamba na uongozi wa serikali wa kata ya Choma kwa kuweza kuvumilia kwa kipindi chote tangia kiwanda kilivyo simama na hata pale alitoa ombi lake la kukufua tena kiwanda waliweza kumsikilliza na hivyo ni jambo la kushukuru.
Lakini pia mmiliki wa kiwanda hicho ndug, Rajan ametoa ombi kwa wakulima wa zao la pamba kuweza kujitaidi kulima zao hili kwa kasi, kwa kuwa kiwanda kinategmea sana zao hili na si zao jingine, hivyo pesa watakayo ilipa toka kwawakulima wana imani nao itarudi pale watakapo wauzia wafanya biashara na ndio kiwanda kitazidi kuendelea.
” Ninafurahi Mbunge Gulamali ameitikia wito wangu kwa kuja na kuona maendeleo ya kutaka kufufua kiwanda hichi hivyo, ni jambo zuri kuona kiongozi akiwa sambamba na wewe na mwenye kutaka maendeleo,
” haitochukua muda tutaaenda kuanza kazi hivyo nina waomba wakulima wa zao hili kuchangamkia fursa kwenye ulimaji kwa kuwa fedha watapata za kuendesha maisha hata ajira pamoja na kukuza uchumi wa nchi yetu, alisema. Rajan.
Hata hivyo Mwenyekiti wa kijiji cha Choma, Ndug, Emmanuel Methew alisema kuwa kitendo kilichofanyika leo cha mbunge kuja kuona maendeleo ya ufufuaji wa kiwanda hiki ni kitu kizuri kutokana ni mikaa mingi kutofanya kazi hivyo wakulima walikuwa wanapata tabu katika zao hili, hata mwishowe kukata tamaa katika kulima zao hili kutokana na kufa kwa kiwanda hiki.
“Kiwanda kufufuliwa tena ni jambo zuri hivyo nina imani kuwa wakulima watarudisha nguvu zao kwa kasi kwenye zao hili la pamba kwakuwa ndio moja ya zao kubwa katika mkoa wa Tabora, alisema Methew

Comments


Popular posts from this blog

DROO YA KLABU BINGWA ULAYA HII HAPA

Nyumba ya Mbunge Kigoma Mjini Zitto Kabwe yaungua moto

Wanawake wasiowaita waume kwa majina yao India

Cristiano Ronaldo kawaonesha watoto wake mapacha leo

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO

Baada ya Kifo cha Mumewe… Zari Akwaa Aibu 5 #Tazama

hali ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu

Emmanuel Mbasha, aweka wazi haya .