LWANDAMILA ALAMBA SHAVU NONO TOKA YANGA

KIROHO safi Yanga imeamua kumuongezea mkataba wa mwaka mmoja kocha wake George Lwandamina raia wa Zambia baada ya ule wa awali kumalizika Julai 16, mwaka huu. Katika mkataba wake uliopita, Lwandamina aliiwezesha Yanga kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita na kuifikisha katika nusu fainali ya Kombe la FA kabla ya kutolewa na Mbao FC ya Mwanza.

Katibu Mkuu wa Yanga, Boniface Mkwasa aliliambia Championi Jumamosi jana mchana kuwa, wameamua kumuongezea mkataba Lwandamina baada ya kuridhishwa na kazi yake.

“Tunaingia mkataba mwingine wa mwaka mmoja na Lwandamina kwani ule wa mwanzo umeisha na sasa kila kitu kipo tayari hivyo muda wowote tena kwa uwazi kabisa atasaini mkataba mpya.


“Tumejitahidi kwa uwezo wetu kuboresha mkataba wake mpya kwa kumuongezea maslahi kidogo ili apate motisha ya kufanya kazi yake ipasavyo,” alisema Mkwasa. Lwandamina alitarajiwa kusaini mkataba huo muda wowote kuanzia jana mchana ili awe na uhakika wa kuendelea kufanya kazi yake kwa uhuru na kujiamini.

Comments


Popular posts from this blog

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO

KENYA :Caroline Odinga akutwa amekufa

mimi nipo sex Lulu diva

mchezaji afariki uwanjani

Mambo 10 ukiyazingatia wewe ni mke bora katika ndoa

Gabo amkana Wema Sepetu

Mabodi aitaka CCM iendelee kufanya sera za ushindani wa maendeleo 

BREAKINGNEWS serikali yamjibu tundulisu