maendeleo ya Tundu lissu mpaka sasa

Lissu anatibiwa jijini Nairobi nchini Kenya mara baada ya kushambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi na watu wasiojulikana, septemba 7 akiwa mkoani Dodoma akitoka kuhudhuria vikao vya Bunge.
Kwa sasa nipo Arusha, ila tangu nilipotoka hivi karibuni Nairobi alikuwa anaendelea vizuri na hali yake inazidi kuimarika na anaendelea na mazoezi kila siku, unajua chumba alichomo kwa sasa ni kikubwa, hivyo anafanya mazoezi humo humo,”amesema Mughwai
Aidha, tangu septemba 7, Lissu hakuwahi kuonekana hadharani hadi oktoba 18 zilipotolewa picha zake na kutumwa kwenye mitandao ya kijamii zikimuonyesha akiwa amelala kitandani na zingine zikimuonyesha akiwa kwenye kiti cha magurudumu.

Hata hivyo, ameongeza kuwa kuhusu kutibiwa nchi za nje, amesema kuwa taarifa ataitoa pale muda utakapo wadia hivyo amewaomba Watanzania kuwa wavumilivu kwani taratibu zinafanyika.

Comments


Popular posts from this blog

wananchi wamshtaki polisi kwakuwanyanyasa

sharti la polepole lapata upinzani

KENYA:Tume Huru ya Uchaguzi yaridhia maombi ya upinzani

Angelina Jolie kuonekana kwenye jarida la ‘Vanity Fair’.

Afisa wa serikali ajinyonga

Viongozi wa G7 waangazia bara la Afrika

UEFA kuendelea kutimuavumbi hii leo

YANGA YASHUSHA STRAIKA WA AFCON